Na Nickson
Mahundi,Njombe.
Waandishi wa habari mkoani Njombe wameungana na wenzao nchini katika kulaani mauaji ya mwandishi mwenzao wa kituo cha runinga cha chanel ten Daudi Mwangosi yaliyotokea Septemba pili katika kijiji cha Nyololo wilayani Mufindi mkoani Iringa.
Akizungumza
na waandishi wa habari mwenyekiti wa muda chama cha waandishi wa habari mkoa wa
Njombe Bw. Bazil Makungu alisema wandishi wa habari mkoani hapa hawaishi katika kisiwa hivyo
kitendo cha kinyama kilichomkuta mwandishi mwenzao Daudi Mwangosi aliyekuwa
mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa Iringa hakitafumbiwa macho.
Bw.Makungu
alisema unyama huo unaweza kumkuta mwandishi yeyeote nchini wakati akitekeleza
majukumu yake iwapo hakutakuwa na umoja na kuungana na waandishi nchini kulaani
mauaji hayo kwa nguvu zote.
“Waandishi
wa habari mkoa wa Njombe tunaungana na wenzetu nchini kulaani mauaji ya
mwandishi mwenzetu Daudi Mwangosi, na kuanzia leo ni marufuku kwa mwandishi wa
habari mkoani hapa kufanya kazi na jeshi la polisi bila tamko kutoka UTPC,
iwapo atatokea mwandishi akafanya nao kazi tutajua huyu si mwenzetu na hataki
ushirikiano na umoja wetu,’’ alisema Makungu.
Aidha
aliitaka serikali kutoa tamko juu ya mauaji hayo ya kinyama ambayo alisema kwa
kawaida hayavumiliki katika taifa hili na ni kitu cha kushangaza ulimwengu kwa
nchi kama Tanzania kutumia nguvu kiasi hicho kuwaua waandishi wa habari.
Hata hivyo
baadhi ya waandishi wa habari mkoani hapa wameshangazwa na kitendo cha mkuu wa
jeshi la polisi nchini IGP Said Mwema kutomsimamisha kazi Kamanda wa jeshi la
polisi mkoani Iringa Michael Kamuhanda ili kupisha tume ya uchunguzi ya mauaji
hayo.
“Tunamshangaa
sana IGP Said Mwema kwa kushindwa kuchukua uamuzi mgumu juu kamanda wa polisi
mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda ambaye ameshindwa kusimamia usalama wa raia na
mali zao na badalayake kuwaua raia wasio kuwa na hatia,” alisema Bw.Makungu.
Itakumbukuwa
kuwa Daudi Mwangosi mpaka mauti yanamkuta alikuwa Mwenyekiti wa chama cha
waandishi wa habari mkoani Iringa (Iringa Press Club) IPC.
No comments:
Post a Comment