Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

January 22, 2016

SHULE YA MSINGI KIBITO WILAYANI LUDEWA YAKABILIWA NA UHABA WA VYUMBA VYA MADARASA.

hili ndilo jengo la shule ya msingi kibito lenye madarasa mawili ambayo wanafunzi walianza kusomea
Haya ndio madarasa mapya ya shule ya msingi kipito ambapo kuanzia darasa la kwanza hadi la saba wanasomea katika vyumba viwili vya madarasa haya

hivi ni vyoo vya shule na walimu wa shule ya msingi Kibito
hivi ni vyoo vya shule na walimu wa shule ya msingi Kibito 
shule ya msingi Kibito
wanafunzi wakipeana zamu za kusomea madarasa hayo yenye vumbi



 mwalimu Mlelwa mmoja wa walimu wa shule hiyo
mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kibito Mwalimu Nikodem Haule shule,shule hiyo ina walimu watatu





Shule ya msingi Kibito katika kijiji cha Madindo kata ya Ludende wilayani Ludewa mkoa wa Njombe emekubwa na uhaba mkubwa wa vyumba vya madarasa hali inayosababisha wanafunzi kuanzia darasa la kwanza hadi la saba kutumia vyumba viwili vya madarasa katika masomo yao.


Shule hiyo ambayo awali ilianzishawa na mwananchi mmoja anayejulikana kwa jina la Aulelian Ngailo Wipata kwa kujenga vyumba viwili vya madarasa kwa kutumia ujenzi wa mianzi na udongo na juu ikiezekwa  nyasi imeendelea kuwa katika mazingira magumu hali iliyo mlazimu mwananchi huyo kujitolea tena kujenga chumba kimoja  cha darasa na ofisi kwa kutumia tofari za kuchona na kuwaacha wananchi wa eneo hilo wakichangia nguvu katika ujenzi wa darasa moja.


Akiongea na mwandishi wa habari hii Bw.Ngailo alisema kuwa kutoendelea kwa shule hiyo mpaka sasa na kusababisha wanafunzi wa madarasa yote kusomea vyumba viwili vya madarasa imesababishwa na uzembe wa Mwenyekiti wa kitongoji ambaye amekuwa nyuma katika kuhamasisha wananchi kufanya kazi ya kimaendeleo katika ujenzi wa shule hiyo.


Bw.Ngailo alisema kuwa awali shule hiyo ilianza kwa kasi katika ujenzi hali iliyopelekea yeye kujitolea kujenga chumba kimoja cha darasa na ofisi ya walimu lakini baada ya kuondoka uongozi uliokuwepo na kuingia uongopzi mpya hali imezidi kuwa mbaya kwani hakuna kinachoendelea shuleni hapo na kuwaacha wanafunzi wakisomea mazingira mabaya ambayo ni aibu kwa wilaya ya Ludewa.


“uongozi ulioingia wa vijana hakuna hata mzee mmoja katika kamati ya ushauli,wanaamua wanavyoona wenyewe kwani Serikali ilileta saruji mifuko miambili lakini hata vyumba hivyo viwili vya madarasa havijasakafiwa na saruji iko stoo tu ikiendelea kuharibika na inamuda wa miaka miwili mpaka sasa,sisi wazee tumeona tuwaache wafanye wawezalo maana tukiwauliza wanadai tunawaingilia”,alisema Bw.Ngailo.


Akijibu tuhuma hizo za wazee Mwenyekiti wa kitongozi cha Kibito ambaye pia ndiye msimamizi wa kazi za kimaendeleo shuleni hapo Bw.Andrea Mgimba alisema kuwa yeye na kamati yake wamejitahidi katika ujenzi wa shule hiyo mpaka hapo ilipofikia nakini yeye siye kikwazo cha maendeleo katika ujenzi wa shule hiyo.


Bw.Mgimba alielekeza lawama Serikalini kuwa imeizira shule hiyo licha ya kuleta mifuko 200 ya saruji na kushindwa kufanyiwa kazi kwa muda wa miaka miwili hivi sasa kwani alisema kuwa kitongoji hicho kila wakazi wachache hali inayosababisha washindwe kufikia malengo katika ujenzi wa vyumba vingine vya madarasa.


Aidha mwalimu mkuu wa shule hiyo Mwalimu Nikodem Haule alikili kuwapo na changamoto nyingi shuleni hapo ikiwepo upungufu wa vyumba vya madarasa na ukosefu wa vyoo vya kisasa kwa matumizi ya walimu na wanafunzi hali ambayo ni hatari kwa afya kwani inaweza kusababisha magonjwa ya mripuko muda wowote.


Mwalimu Haule alisema kuwa shule hiyo imekuwa ikisaidiwa kwa kiasi kikubwa na diwani wa kata hiyo mh.Mseya ambaye ameahidi kujenga vyumba vingine vya madarasa ili kuwanusuru wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo ya msingi kipito.


Mwisho.

No comments: