Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

November 14, 2015

MRITHI WA DEO FILIKUNJOMBE APOKELEWA KWA MAANDAMANO MAKUBWA LUDEWA WAMTAKA KUFANYA ALIYOYAFANYA HAYATI.



 

 huyu ndiye Deo Ngalawa mgombea ubunge tiketi ya ccm jimbo la Ludewa
 Deo Ngalawa akipokelewa kwa maandamano Ludewa mjini



Deo Ngalawa akisalimiana na katibu tawala wa wilaya ya Ludewa Bw.Ulaya


 Ngalawa akiwa katika Maandamano



 maandamano yakiendelea kuelekea ofisi za ccm Ludewa mjini
 Deo Ngalawa akiwa katika ofisi za ccm wilaya ya Ludewa


Mgombea ubunge kwa tiketi ya chama cha mapinduzi(ccm)Deo Ngalawa jimbo la Ludewa ambaye ni mrithi wa hayati Deo Filikunjombe amepokelewa kwa maandamano makubwa ya kumuunga mkono na wanachama wa vyama mbalimbali vya siasa wilayani hapo wakati akitokea jijini Dar es Salaam.

Mapokezi hayo makubwa yamekuja  baada ya mwenyekiti wa kamati kuu ya CCM rais mstaafu Dr.Jakaya Mrisho Kikwete kumpitisha rasmi Bw.Ngalawa kuwa mgombea wa nafasi ya ubunge kwa jimbo ambapo katika kura za maoni Bw.Ngalawa aliibuka mshindi dhidi ya wapinani wake tisa ambao alichuana nao vikali kuisaka nafasi hiyo.


Licha ya kuwa mgombea huyo anatoka chama cha mapinduzi lakini ameungwa mkono na vyama vingine vya siasa kutokana na hali halisi kuwa Bw.Ngalawa hakuwahi kuwa na kashfa yoyote wa kundi hivyo amekuwa ni mfano katika jamii ya Ludewa na anauwezo wa kufuata nyayo za hayati Filikunjombe kimaendeleo kwani alishaitendea makubwa wilaya ya Ludewa kwa kushirikiana na aliyekuwa mbunge wa jimbo la Ludewa.


Akiongea katika maandamano hayo jana yaliyoanzia shule ya Sekondari Chief Kidulile na kumalizikia ofisi za ccm wilaya Bw.Titus Haule ambaye ni mwanachama  wa chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) alisema kuwa wameamua kumuunga mkono Ngalawa kutokana na ukweli kwamba hana ubaguzi pia amefanya makubwa ndani na nje ya Ludewa kimaendeleo.


Bw.Haule alisema kuwa kamati kuu ya ccm imetumia busara kulipitisha jina la Ngalawa kwani amekuwa ni msaada mkubwa katika jamii bila kubagua itikadi za vyama au dini mfano mzuri ni ujenzi wa chuo cha ualimu kata ya Lupingu ambapo mpaka sasa majengo yamesha kamilika bado ufunguzi pia ujenzi wa chuo cha Afya Ludewa Mjini ambapo ujenzi unaendelea vizuri na hivyo vyote ni pesa yake mfukoni.



Alisema richa ya ujenzi wa vyuo hivyo kwa pesa yake kama mwanaludewa pia ametoa misaada ya mashine za ukamuaji wa mafuta ya Alizeti pia aliweza kununua magari ya usafiri wa abilia na kuyapeleka maeneo magumu ambaye wananchi wa vijiji hivyo walikuwa wakitembea kwa miguu kwa zaidi ya kilomita 35 kufuata huduma za  kijamii makao makuu ya wilaya.


“Sisi hatujali itikadi za vyama katika wilaya yetu tunachokiangalia ni mtu mpenda maendeleo hivyo tunamuunga mkono kwa asilimia zote Ndalawa kama tulivyo muunga mkono hayati Filikunjombe kutokana na ukweli usiopingika kuwa wote ni majembe katika maenendeleo pia wenzetu wa ukawa baadhi yao walisherekea kifo cha Filikunjombe jambo ambalo limewakera wanaludewa hali inayopelekea kila tukipita mitaani tuonekane wabaya”,alisema Bw.Haule.


Bw.Haule aliwataka wanaludewa kumuunga mkono Bw.Ngalawa ili kuweza kukamilisha mambo mbalimbali ya kimaendeleo ambayo yaliachwa na hayati kwani hakuna mtu mwingine wa kuyaendelea hayo zaidi ya Ngalawa ambaye tokea awali amekuwa akionesha kuleta maendeleo Ludewa.


Aidha Deo Ngalawa ambaye ndiye jina lake limepitishwa na kamati kuu ya ccm kuwa mgombea wa ubunge jimbo la Ludewa alisema kuwa mchakato ndani ya chama ulikwisha hivyo kilichobaki ni kuyavunja makundi na kuwa kitu kimoja katika suala zima la maendeleo wilayani Ludewa.


Bw.Ngalawa alisema kuwa atakamilisha mipango ya hayati Filikunjombe na kumuenzi kwa kuleta maendeleo ya haraka hivyi hata waangusha wanaludewa katika maendeleo jambo la msingi ni ushirikiano mzuri ambao utaleta nguvu ya pamoja kwani yeye peke yake hawezi kufanikisha maendeleo hivyo aliwaomba wananchi kuungana bila kujali itikadi za vyama na dini wala kabila.


Naye katibu wa ccm Ludewa Bw.Rusiano Mbosa aliwataka wananchi kuhakikisha Bw.Ngalawa anapata ushindi wa kishindo katika uchaguzi unaotarajia kufanyika hivi karibuni kwani kwa kufanya hizo wanaludewa watakuwa wamemuenzi hayati Deo Filikunjombe ambaye alikuwa mpiganaji ndani ya chama chake cha CCM.


MWISHO.

No comments: