Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

July 22, 2015

WANANCHI LUDEWA WAWAADHIBU WAGOMBEA UBUNGE WANAOMPINGA FILIKUNJOMBE Uongozi wa ccm wampangia Filikunjombe kuwa wamwisho kujieleza mikutanoni.

wananchi wa kata ya milo wakiwasikiliza wagombea ambapo mgombea wa kwanza alikuwa Filikunjombe na baada ya kumaliza kujieleza walianza kutawanyika


 waha ndio wagombea ubungea jimbo la Ludewa kwa tiketi ya CCM wakiwasalimia wananchi
Kutoka kulia anayeandika ni Mhandisi Zefania Chaula,katikati ni Kampen Jacob Mpangala na kushoto mwenye jaketi ni Deo Filikunjombe

wananchi wa kata ya Lugarawa wakianza kutawanyika baada ya Filikunjombe kumaliza kuongea
 wananchi wakitawanyika mkutanoni na kuelekea makwao na kuwaacha wagombea wengine wakiwa bado hawaja jieleza



WANANCHI wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe wameanza kuwaadhibu wagombe wanaowania nafasi ya Ubunge na wanaompinga Filikunjombe kwa kuwaacha peke yao katika viwanja vya mikutano pale anapomaliza kujieleza Deo Filikunjombe na kujibu maswali ya wananchi wanapohitaji ufafanuzi.


Hali hiyo imeanza kujitokeza juzi katika kata ya Ludende,Milo na Lugarawa katika mikutano inayoitishwa na chama cha mapinduzi ili kuwanadi wagombea watatu wa chama hicho kwa wanachama ili kuweza kupiga kura za maoni ambazo zitampitisha mgombea mmoja wa ccm ambaye atapambana na wagombea wa vyama pinzani.


Katika jimbo la Ludewa ndani ya chama cha mapinduzi wamejitokeza wagombea wawili wakipambana na mgombea aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo wagombea hao ni Mhandisi Zefania Chaula,Kapten Jacob Mpangala na Deo Filikunjombe ambapo hali imekuwa mbaya zaidi kwa wapinzani wa Filikunjombe kwani anapopangwa kuanza kujieleza Filikunjombe wagombea wengine hubaki bila watu na kujikuta wakibaki wao na viongozi wa ccm wilaya.


Mmoja wa wananchi ambao walitoka katika mkutano wa hadhara katika kata ya Lugarawa baada ya Filikunjombe kumaliza kujinadi kwa wananchi Bw.Yusto Mgimba alisema kuwa wananchi wamekuwa na shauku ya kumsikiliza Filikunjombe na wamekuwa na imani naye hivyo hawana mpango wa kuwasikiliza wengine kwani hawajulikani kwa wananchi.


Bw.Mgimba alisema kuwa Filikunjombe bado anakubalika na wananchi wa wilaya ya Ludewa kwani maendeleo na ahadi alizoziahidi mwaka 2010 amezitekeleza pia wanafuatilia kazi anazozifanya awapo Bungeni za kuwatetea wananchi wake hivyo hakuna sababu ya kubadirisha mbunge kama miaka mingine.


“tunawashangaa wagombea hawa wengine wanavyotueleza watafuatilia miradi ya chuma cha Liganga na makaa yam awe ya Nchuchuma na ujenzi wa viwanda vyake wakati kwa macho yetu tumemuona na tumemsikia akifunga Bunge  rais wetu Jakaya Mrisho Kikwete akisema kuwa mwaka huu atakuja kuweka mawe ya msingi ya ujenzi wa viwanda hivyo sasa wao watafuatilia wapi wakati kazi hiyo sisi wananchi tulimtuma Filikunjombe na majibu tumeyapata?”,alisema Bw.Mgimba.


Bw.Mgimba alisema kuwa wananchi hawaoni sababu ya kuendelea kuwasikiliza hao wengine wasiowajua hivyo wakishamsikiliza mbunge wao ambao wanamkubali jembe lao wanatawanyika kwani wanajua watadanganywa tu na hawa wengine kutokana na ukweli kwamba hawana jipya la kuwafanyia wananchi.


Aidha msimamizi wa mchakato huo wa kumpata mgombea mmoja wa chama cha mapinduzi ambaye ni Mnec wa wialaya ya Ludewa mzee Hilaly Nkwera alisema kuwa mchakato unakwenda vizuri na hauna kasoro kwani wagombea wote wametulia na itabidi wakubali matokea hata kama baadhi hawakubaliki na wananchi.


Kuhusu wananchi kuondoka katika mikutano baada ya Filikunjombe kumaliza kijieleza Mzee Nkwera alisema kuwa suala hilo lipo na inashindikana kuwazuia richa ya kuwa wasimamizi wamekuwa wakitoa angalizo kwa wananchi kutoa ondoka lakini imekuwa shida hivyo imebidi wagombea wote wakubadliane kila mkutano Deo Filikunjombe awe wa mwisho kujieleza ili kuepusha hali hiyo.


Mzee Nkwera alisema kuwa makubaliano hayo yanaweza kusaidia kwa upande Fulani ili wagombea wengine wapate kusikilizwa sera zao kwa wananchi kwani bila kufanya hivyo hali itakuwa ni ile ile ya awali ya wananchi kutawanyika baada ya kumsikiliza Filikunjombe na kuwaacha wagombea wengine bila wasikilizaji.


Mwisho.

No comments: