Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

January 25, 2015

MATUKIO YA UHALIFU NJOMBE YAONGEZEKA KWA 1.65% MWAKA 2015 UKILINGANISHA NA MWAKA 2014.



Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe SACP Fulgency Ngonyani  .

Na Michael Ngilangwa  NJOMBE

Jeshi La Polisi Mkoani  Njombe Limetoa Taarifa Ya  Uhalifu Wa Makosa Ya Jinai Kwa Mwaka 2013/2014 Kuwa Yameongezaka  Kwa Asilimia 1.65  Tofauti  Na Mwaka 2013 Ambapo  Kulikuwa Na Jumla Ya Matukio Ya Uhalifu Wa Makosa Ya Jinai 1090 Ambapo Kwa  Mwaka 2014 Yamekuwa  11,008 Ikiwa na Ongezeko la Matukio 18.



Akizungumza Na Waandishi Wa Habari Akiwa Katika Ukumbi Wa Polisi Mkoa Wa Njombe Kamanda Wa Jeshi La Polisi Mkoa SACPFulgence Ngonyani  Ameyataja Baadhi Ya Matukio Yaliopungua Na Kuongezeka Kwa Kipindi Cha Mwaka 2013/2014 Kuwa Ni Pamoja Na  Matukio Ya Mauaji  Ambayo 2013 Yalikuwa 103 Na Mwaka 2014 Yalikuwa 94.


Kamanda Ngonyani Amesema Kuwa  Matukio Ya Unyang'anyi Wa Kutumia  Silaha Mwaka 2013 Yalikuwa 6  Na Mwaka 2014 Yameripotiwa  Matukio Saba,Unyang'anyi Wa Kutumia Nguvu  Yalikuwa 64 Mwaka 2013 Na Mwaka 2014 Yalikuwa  29 Huku Upatikanaji Wa Silaha  Mwaka 2013 Yakiwa Mawili Na 2014  Yakiongezeka Hadi Kufikia Matukio  5 .

Akitoa Taarifa Ya Makosa Ya Usalama Barabarani Yaliyo tokea Kwa Kipindi Cha Kuanzia Mwaka 2013 Hadi 2014 Amesema Ni Makosa 14401 Yaliyo Ripotiwa Kipindi Cha Mwaka 2013 Na Mwaka 2014 Ni Makosa 20564 Ambapo Ongezeko Lake Ni
Makosa 6163.

No comments: