Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

August 29, 2014

RIWAYA; MAMA YANGU MUUAJI




MTUNZI; Moringe Jonas


MAWASILIAANO; Jonasymoringe@gmail.com

SEHEMU YA TATU


KWA WASOMAJI WAPYA;


Delphine anashuhudia wazazi na ndugu zake wakiuawa kikatili na watu wa kabila tofauti na lake nchini Rwanda  kupitia nafasi  kitundu kidogo kilichokuwa chooni alipoelekea mara tuu  baada ya kuamka.Anaamua kukimbia ambako hakujua alikoelekea zaidi ya kupotelea  katika msitu mkubwa uliokuwa mashariki mwa nchi ile uliokuwa ukiziunganisha nchi za Rwanda ,Burundi na Tanzania ambako anaokotwa na watu walioenda kutafuta ngozi ya joka lililokuwa humo kwa kile kilichodaiwa wangepata utajiri.


 Joka hilo la ajabu linasababisha vifo vya baadhi yao kiajabu ajabu hali iliyowafanya watu wale  kupoteana baada ya joka lile kuuawa lakini baadaye linajitokeza , safari hii watu wakionekana kuliabudu.

 Baada ya safari hiyo iliyokuwa na mikasa ya ajabu iliyopelekea   pia kifo cha  mganga aliyewatuma  kuifuata Ngozi hiyo   kinawashtua na kulivuruga kabisa kundi lile la marafiki na kubadili kabisa mfumo wa maisha wa watu wale.


  Miaka ilipita hatimaye Delphine anakuwa binti mkubwa aliyeanza  kuwavutia  wavulana wa rika lake na hata wakubwa baada ya malezi aliyoyapata kutoka katika jamii ya akina Mwita ambaye alimuokoa kule porini.Lakini jambo la ajabu linatokea katika maisha yake ya kujifunza ukunga   ambapo alitakiwa kufanyiwa tohara kama jamii ile ilivyomtaka. Anakimbilia kwa Mwita ambaye alimwona kama  mzazi wake huko nako anagundua kuwa malengo ya kulelelwa yalikuwa kuolewa na Yule baba jambo limfanyalo  akimbilie mbugani kulikokuwa na hatarui kubwa ya kuliwa na wanyama wakali.


  Kwenye kibarabara kisichoeleweka  mbugani anashtushwa na sauti ya kutisha ambayo kadiri muda ulivyopita iliongezeka na kumfanya akose la kufanya.

SONGA NAYO………..


  Gari dogo la kitalii lilionekana kwa mbali kilima na kumfanya Delphine apate tumaini jipya kwani akili yake ilimwaminisha ilikuwa ni sauti ya simba.Alijiweka vizuri kuomba msaada lakini alama ya michilizi ya mkojo uliotokana na hofu zilishindwa kufichika.


‘’We binti huogopi hapa porini?’’aliuliza  baba mmoja mara baada  lile gari kusimama.

‘’Nina matatizo makubwa hapa nilipo baba yangu’’Aliongea Delphine akiangalia garini ambako kulikuwa na watu wasabi huku dereva aliwa ni mwafrika pekee wengine wote wakiwa wazungu.

‘’Haya panda gari haraka tukupeleke sehemu salama’’Alimrisha Yule baba akianza kuelekea garini. 

  Gari dogo la kitalii lilionekana kwa mbali kilima na kumfanya Delphine apate tumaini jipya kwani akili yake ilimwaminisha ilikuwa ni sauti ya simba.Alijiweka vizuri kuomba msaada lakini alama ya michilizi ya mkojo uliotokana na hofu zilishindwa kufichika.


‘’We binti huogopi hapa porini?’’aliuliza  baba mmoja mara baada  lile gari kusimama.

‘’Nina matatizo makubwa hapa nilipo baba yangu’’Aliongea Delphine akiangalia garini ambako kulikuwa na watu wasabi huku dereva aliwa ni mwafrika pekee wengine wote wakiwa wazungu.


‘’Haya panda gari haraka tukupeleke sehemu salama’’Alimrisha Yule baba akianza kuelekea garini. 

  Delphine alipanda kwenye lile gari la kitalii na kukaa kwenye moja ya siti zilizokuwa garini akiwaacha wale wengine wakiwa wamesimama wakiendelea kupiga picha  wanyama na miti iliyoonekena kama muhimu sana kwao kwa wakati ule kwani ndicho kilichowapeleka kule porini.


 Hakukuwa na mzungu hata mmjoja aliyejishughulisha na Yule msichana zaidi ya kumsikiliza  Yule mtu aliyekuwa akiwaeleza kuhusu  mambo mbalimbali waliyoyaona  kila walipopita.

 Katikati ya mazungumzo hayo ambayo  lugha ya kifaransa ikitawala , ambapo maneno machache tuu yalipata maana kwenye ubongo wa Delphine amabaye alishtuka kila alipowaona simba. Aliwaza kama angeendelea kutembea mle mbugani peke yake  kama angefanikiwa  kutoka salama kwenye mbuga ile iliyokuwa kubwa sana Afrika  Mashariki.


Taswira ya ndugu zake wakiuawa ilijirudia akilini mwake na kujikuta akitoa machozi na hakujua  sababu iliyomfanya awakumbuke wakati ule kwani alikuwa hajawakumbuka kwa muda mrefu kufikia hatua ya kutoa machozi.Ilitokea mara chache sana  kwake kuwalilia wazazi wake waliokuwa wamepoteza maisha miaka  zaidi ya kumi iliyopita na kila alipofikia hatua hiyo alitamani kurudi  tena Rwanda kulipiza kisasi juu ya mambo yaliyotokea  kipindi kilichopita.Aliwachukia sana watu wale akiapa kutowasamehe  milele wale watu kwani aliamini hata kwa toba ipi wasingesamehewa  hata  na Mwenyezi Mungu.


Alijua wao ndio waliosababisha awe katika hali ile ya kukimbia kimbia , tena akiwakimbia wanadamu wenzake ambao kila mmoja hakuwa nania njema kwani wakati akikimbia kukeketwa anakutana na jambo jipya la kutaka kuolewa na  mwanaume ambaye kwake alikuwa ni kama baba yake.Yote hayo yalitokana uhasama wa kikabila uliochochewa na siasa chafu nchini mwake, alitamani kuona siku watu wale wakiadhibiwa kwa mateso makali  ambayo huenda  yangekuwa ni pozo la moyo wake.


  Gari la kijani aina ya LAND CLUISER lilisimama mbele ya jengo moja ambalo  lilionekana ndiyo mwisho wa safari ya watu wale waliokuwa  garini waliomtaka Delphine ashuke  pamoja nao.

Walipofika ndani ya jengo lile waliletewa chakula huku Delphine akihimizwa na kila mmoja kula na baada ya kula alipewa mavazi ambayo alitakiwa kuyavaa baada ya kuoga kwani mavazi aliyotoka nayo kijijini yalikuwa kmachafu sana. Mavazi yale yalifanamna na mavazi waliyovaa wafanyakazi waliokuwa wakifanya kazi ya upishi katika nyumba ile iliyokuwa  ni hoteli ya kitalii, jambo lililomshangaza Delphine kwani awali aliamini kuwa ni watalii tuu sasa ilikuwaje wampe mavazi yaliyokuwa sare za wapishi  wa iile hoteli ya kitalii.


‘’Unaitwa nani?’’Lilikuwa ni swali la kwanza alililoulizwa  Delphine mara tuu alipoketi kitini  baada ya kuoga na  kubadili zile nguo zilizomfanya  aonekane kama  mmoja wa wapishi wa ile  Hoteli.

‘’Delphine Mwita’’alijibu huku akionekana  kuwa na uoga wa ajabu kwani alijikuta akiamua kuwadanganya wale watu  ili apate msaada.


‘’Umetokea wapi  na kwa nini ulikuwa pale porini?’’Aliuliza maswali  mfulizo Yule mtu huku akionekana kuwasikiliza sana  na kuwaelekeza  wale watalii wa kizungu .

‘’Nimetokea Mugumu  huko walitaka wanikekete na  kunioa katika umri huu mimi yatima jamani’’Aliongea Yule binti akitoa nkilio cha hisia kilichowafanya wale watu wamhurumie sana  kabla hata ya kuelekezwa maana ya alichokiongea na yule aliyeonekana kama mkalimani  wao.


 Baada na maelezo mengi yaliyojaa uongo uliokuwa  wa kiwango cha juu kufikia hatua ya kumtoa machozi mama mmoja ambaye alionekana naye  kama ana mamlaka Fulani kwenye ile hoteli  kutoa machozi akimtaka amshukuru sana mungu kwa  kumwepusha na mauti akiwa  mbugani , mbuga ambayo ilikuwa na  wanyama wengi  hatari kwa maisha ya wanadamu hata wanyama wenzao.


 Baadaye alitakiwa kulala na mmoja wa wapishi wa hoteli ile huku wakiahidi  kumpa msaada alioumba ambao ulikuwa ni kuwa mbali juu ya watu wale waliotaka kumfanyia mam,bo ambayo hakupenda kabisa yatokee kwake.

  Uchovu na kilio cha jioni ile vilimfanya Delphine apate usingizi mapema sana mara tuu alipojitupa kitandani akimwacha  mwenzake aliyetakiwa kulala naye akihanagaika hangaika mle ndani na pilika zilizokuwa hazina maana, mara akashike chanuo mara ajaribu gauni mara akwangue kucha za miguu  ili mradi tuu hatulii.Usiku wa manane Delphine alishtuka kutoka usingizini baada ya kuota ndoto Fulani ya kutisha ambayo Marehemu  Mama yake alimtokea ndotoni  akimwambia kuwa wale watu aliokuwa nao hawakuwa wema hata kidogo ajitahidi kuondoka pale mapema sana kabla mabo mabaya hayajamtokea.


 Alipoangalia Pembeni yake ambapo Yule mwanamke aliyeambiwa angelela  naye  hakuona chochote zaidi ya shuka lililokuwa kimekunjwa   kana kwamba kakukuwa na mtu aliyelala pale.

‘ Aliogopa’, hasa kutokana na ile ndoto ambayo ilimhusisha mtu aliyefariki miaka mingi iliyopita , tena  hakuwahi kumwota hata siku moja tangu alipouawa kinyama na wale watu.Alianza kupata hofu juu ya wale watu ambao hakujua  walikuwa na kazi gani japo walionekana kama watalii lakini walikuwa  na mamlaka sana tofauti na  walivyokuwa watalii wengine waliokuwa pale hotelini.


Akiwa katika kutafakari juu ya mambo hayo alishtushwa na sauti ya hatua zilizokuwa zikionekana zikielekea  katika chumba kile alichokuwa amelala, wazo la haraka lilimjia akijamini kuwa alikuwa ni Yule rafiki yake waliopangwa  kulala pamoja.


Bila kutarajia alijikuta anachukua uamzi wa kusimama na kujificha nyuma ya kabati  la nguo lililokuwa  mle ndani , na Yule mtu alipoingia alikuwa ni mtu ambaye alimfanya ashindwe kuelewa sababu  iliyompeleka pale ndani muda ule.

  Alikuwa ni mmoja wa wale watu aliosafiri nao wakitokea Mbugani akiwa ndiye Dereva wao , ambaye moja kwa moja alienda kitandani kujilaza na kujifunika ile shuka iliyokuwa imekunjwa pale pembeni ya alipolala Delphine .


Akiwa nyuma ya ile kabati ndogo Delphine alitetemeka sana baada ya kuona Yule mtu akiamka na kuanza kuangaza huku na huko mle ndani kabla ya kutoka nje ya kile chumba.Yule mtu alirudi muda mfupi baadaye akionekana bado akitafuta kitu  mle  ndani  jambo ambalo Delphine alilinganisha na ndoto aliyokuwa ameiota.


ITAENDELEA……………

Je , Yule mtu alifuata nini ?

Yupi ni mama muuaji?








No comments: