Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

July 28, 2014


RIWAYA;MAMA YANGU MUUAJI

MTUNZI;Moringe john Mhagama

SEHEMU YA KWANZA

Kila mtu aliyefika pale nyumbani alionekana kunishangaa kwa mwonekano niliokuwanao,sikuonekana kabisa kushughulika na msiba ambao mimi ndiye mfiwa pekee wa moja kwa moja niliyekuwepo pale.

Hakukuwa na ndugu mwingine aliyekuwepo zaidi ya marafiki wa marehemu mama yangu ambaye katika maisha yangu yote niliyoishi naye sikuwahi kuwaona ndugu zake wengine hadi masaa machache kabla ya kifo chake ambapo aliniambia ukweli si tuu ulimuumiza yeye bali hata mimi uliniumiza sana na kufanya niamini kuwa mama yangu alikuwa muuaji ,kitendo ambacho sina hakika kama mungu alimsamehe kwani hata kifo chake kilikuwa cha kujiua. 

‘’Yule kijana kama hajafiwa yaani hana habari kabisa’’ilisikika sauti ya mama mmoja ambaye alionekana kuumizwa na tabia niliyooneshwa.
‘’Huwezi jua mama ni mama anaweza kuwa anaumia kwa ndani’’Alijibiwa na mama mwingine wakati huo idadi ya watu ikizidi kuongezeka kwani marehemu mama yangu kabla ya kifo chake alikuwa ni miongoni mwa watu waliokuwa na marafiki wengi nadhani kutokana na tabia yake ya kucheka na kila mtu aliyokuwa nayo .

‘’Hapana huyu kijana amezidi haiwezekani mtu umefiwa na mama yako mzazi halafu masaa yote unacheza na simu yako tuu’’Alidakia mama mwingine ambaye kabla ya kifo cha mama alikuwa akija mara kwa mara pale nyumbani. 

‘’Labda anawasiliana na ndugu zake awape taaarifa za msiba’’Ilisikika sauti nyingine kwani kitendo change cha kuonekana nimevaa ‘earphones’ ziliwapa uhuru wa kuongea kwa sauti ya juu wakiamini sikusikia chachote ambacho walikiongea.

‘’Ana ndugu huyooo mama yake hawajui si wa upande wa baba si wa upande wa mama’’Yule mama aliyeanzisha majadiliano aliongea akionekana kuijua historia yetu huku maneno yake yakinifanya niondoke mahali pale na kuingia chumbani kwangu huku nikikumbuka yale aliyoniambia mama yangu nikijaribu kuyapima kama yalikuwa na ukweli wowote. 


Nilikumbuka kauli ya mama kuwa aliamua kujiua kutokana na mambo kumwelemea na hatari iliyokuwa mbele yake kukosa njia ya kujiokoa.Sikutaka kabisa kuamini kama aliyoyaongea yalikuwa ya ukweli au kulikuwa na jambo lingine lililojificha hadi kumpelekea mama yangu ndugu yangu wa pekee niliyemfahamu hapa duniani. 

Nakumbuka tofauti na siku nyingine mama yangu alirudi mapema siku ile akiwa kwenye hali tofauti na niliyomzoea siku zote kwani alikuwa na tabia ya kuingia pale nyumbani kwa matani na vichekesho vya hapa na pale kila alipofika.

Siku ile baada ya kutupa kibegi chake kochini alikaa chini na kuniomba nimpe chai jambo ambalo nililifanya kwa haraka kwani haikuwa kawaida kwake kuwa vile hivyo hali iliyonifanya niamini kuwa huenda alikuwa anaumwa. 

‘’Mwanangu usiogope haya ni maisha ya kawaida unaonekana kumwogopa mama yako usimwogope leo ameamua kuwa mkali kama baba yako’’Aliongea mama yangu akikoroga sukari kwenye chai aliyoimimina huku akijilazimisha kutabasamu tabasamu ambalo lilishindwa kuishi usoni pake hata kwa sekunde kumi na kicheko chake kikiishia kooni na kuniongezea hofu na si kunitia tumaini tena. ‘’

Hapana mama utakuwa unaumwa au kuna watu wamekuvuruga huko kazini kwako ‘’Niliongea kwa masikitiko makubwa kwani mara nyingi ilikuwa kawaida kunieleza jambo lililomkera huko kazini kwake. ‘’Hapana mwanangu nataka nikuambie kitu kimoja muhimu sana ‘’Sauti yenye mikwaruzo ilisikika na kunifanya nimsikilize kwa umakini mkubwa. 

‘’Kama kitu muhimu ndio uwe hivyo mama?’’Niliongea kwa hofu ambayo mama yangu aliigundua na kujifanya kucheka kicheko ambacho ni kama kilikuwa na ugonjwa kwani hakikuendana na hali niliyoiona usoni mwake. ‘’

Ndiyo najua hunifahamu vizuri mwanangu nataka unijue mama yako nilivyo na sababu ya mimi leo kuwa hivi maisha haya hayaeleweki naweza hata nikafa hata usijue historia yako’’Aliongea mama yangu na kuchukua kikombe cha chai kisha kunywa funda moja.

‘’Kwani si ulisha niambia juu ya maisha yako mama kwa nini unapenda kukumbuka mambo yakuumizayo tumepata nafasi ya kubaki hai basi tuendelee kuishi huku kazi yako Mungu kakubariki kuifanya na inatufanya tuishi kwa hiyo hakuna ulazima wa sisi kendelea kulalamika…..’

’Uchungu ulionishika juu ya kumbukumbu ya maisha yetu zilinifanya nishindwe kabisa kuvumilia na kujikuta naanza kulia bila kujua historia ya maisha yake iliyo ya kweli ambayo kila nikiikumbuka inanifanya niseme’’ MAMA YANGU MUUAJI’’.
*******

Machi 27 1994 RWANDA Chuki baina ya makabila mawili makubwa nchini Rwanda ilizidi kuongezeka huku watu wa kila kabila wakiamini kuwa wenzao kutoka kabila lingine ni watu wabaya na wasiostahili kuishi jambo lililozidi kuchochea na kuongeza mauaji yale.

Wahutu waliwaona Watutsi ni watu wabaya kwao huku upande wa pili ukiamini kinyume chake na mauaji yakizidi kuongezeka kila siku huku kila usiku ukiwa ni usiku wa mauaji ambako watu wengi walikuwa wakipoteza maisha kwa mateso makubwa.

Umoja wa Mataifa na nchi nyingine zilionekana kulalamikia tukio lile huku vyombo vya habari vikihamishia kamera zao na wandishi wao kwenye nchi hiyo ndogo ambayo ilikuwa kabla ya vita vya kwanza ya Dunia ilikuwa ni sehemu ya Tanganyika.

pamoja na nchi jirani ya Burundi na habari kufikia hata idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza(BBC) kuandaa kipindi maalum cha mambo yaliyoendelea nchini humo wakiwahoji wanachi mbalimbali huku wakiongea na viongozi wa Serikali ambao nao hisia zao za ukabila zikijionesha kila walipohojiwa.

Wakati hayo yakiendelea katika kijiji kimoja kilichokuwa Mashariki kabisa mwa nchi ile mtoto mmoja alikuwa akitetemeka kwa hofu baada ya kushuhudia wazazi wake wakiuawa kinyama kupitia kitundu kidogo kilichokuwa chooni kwani baada tu ya yeye kuingia chooni watu wenye silaha za jadi waliivamia familia yake iliyokuwa na wazazi wake na ndugu zake wawili wa kike na wakiume na kuwaua kikatili


Alisubiri hadi wale watu walivyoondoka na kuanza safari ya kutoroka kijiji kile huku akiwa hajui ni sehemu ipi iliyokuwa salama kwake.Harufu ya damu za wazazi na ndugu zake ilisikika kila alipokumbuka kilichomfanya atoe machozi kila wakati.

Safari isiyokuwa na mwongozaji ilipitia katikati ya msitu mmoja ambao aliusikia katika hekaya za wazazi wake kunwa ni msitu uliokuwa na maajabu mengi na lilikuwa ni jambo la kawaida kupotea kwenye msitu huo.

Japokuwa alikuwa muoga lakini kitendo cha kushuhudia vifo vya wazazi wake kilimwongezea nguvu ya kusonga mbele akiepuka mauaji yale akiwa katikati ya msitu ule binti huyo mwenye umri wa miaka mitano anazidiwa na njaa na kupoteza fahamu kutokana na njaa aliyokuwa nayo. 

Baada ya masaa matatu kuna sauti za watu ambao walionekana kuwa makini kwa kila hatua waliosogea,wakimvizia nyoka mmoja mkubwa ambaye walikuwa wamemfuatilia kwa umbali wa zaidi ya kilometa kumi wakitaka kumuua ili tuu wapate ngozi yake ambayo ilionekana wakiihitaji sana kwa kipindi kile.

Hawakujua kabisa uelekeo wa nyoka Yule ulikuwa ni kufuata chakula ambacho alihisi uwepo wake mahali pale.Chakula hicho hakikuwa kingine zaidi ya mwili wa Yule binti aliyeyaacha magofu yakiwa na mizoga ya watu waliouawa na binadamu wenzao kisa kikiwa ni chuki tuu za ukabila japo kwa wakati ule aliambiwa tuuwatu fulai ni wabaya lakini hakuwahi kufikiria kuwa wanaweza kufikia hatua ya kuwaua ndugu zake.

Kwa kuwa jioni ilikuwa imekaribia watu waliokuwa wakimwinda Yule nyoka ili tuu wamuangamize ii wapate walichokitaka bila ya kuvunja masharti ya mganga wao aliyewataka wampelekee ngozi ya nyoka huyo ambaye alikuwa hajatoka kumla mtu ili dawa yao ifanye kazi vizuri na sharti gumu kabisa lilikuwa ni kumuua Yule saa kumi na mbili na nusu jioni vinginevyo wasingepata walichokitaka.

Lakini ghafla walishtuka baada ya kumwona nyoka Yule akiongeza mwendo na kuwafanya wahisi kuwa huenda aligungua kuwa alikuwa anafuatiliwa ama kuna chakula mbele yake kwani nyoka huyo ilisemekana alikuwa akila nyama hasa za watu na hiyo ndiyo sababu ya watu wengi kuuogopa msitu ule.

na mara chache alikuwa akivamia vijini na pwani ya ziwa Tanganyika na kuwavamia wavuvi,Ilisemwa kuwa nyoka huyo alikuwa ni mungu wa kabila Fulani nchini Burundi lakini makao yake makuu yalikuwa ni katika msitu huo uliokuwa umepita kuanzia Burundi hadi sehemu ya Rwanda.

Hatimaye nyoka Yule alikuwa hatua mbili kabla ya kuufikia mwili wa msichana Delphine Daniel ambaye alikuwa amepoteza fahamu huku sababu kubwa zikiwa ni njaa na uchovu wa safari ya kutwa nzima
‘’Shiii……’’ilisikika sauti iliyomshtua Yule nyoka wakati huo zilikuwa zimebaki dakika kama kumi ufike muda walioambiwa na mganga wao kuwa walitakiwa kumuua Yule nyoka na kumfanya Yule nyoka aachane na chakula kilichokuwa mbele yake na kuwageukia maaadui wake ambao hakujua walimfuatilia kwa takribani masaa matatu yaliyopita.

Mapambano ya mikuki na mishale kutoka kwa watu watano waliokuja pale kwa lengo moja tuu la kumuua Yule nyoka saa kumi na mbili na nusu.Lakini walitakiwa kumzuia tuu asiwadhuru ili dakika kumi zilizobaki ndipo wammalize lakini sumu kali alizozitema ziliwafanya wawili kati yao wapoteze uwezo wa kuona.

Mate ya sumu yalifika moja kwa moja machoni mwao na wale wengine kupata muwasho uliowapunguzia umakini kwani hawakujua kabisa kama mwenzao aliyewekwa kwa ajili ya kuwasomea muda alikuwa amepoteza uwezo wake wa kuona hivyo walipambana tuu akisubiri wakati ufike.

‘’Mhh muda haujafika?’’Aliuliza mmoja wao huku akijikuna shingoni kwake baada ya kutemewa mate yenye sumu na Yule mtu.
‘’Jamani sioni’’Alijibu Yule msoma muda akijaribu kumpa saa Yule mwenzake lakini kabla hata ya kuipokea ile saa aliona ile saa ikirushwa mbali na mkono wake ukikoswa koswa na sumu iliyorushwa na Yule nyoka ambaye tofauti na nyoka wengine alitumia sumu kumdhibiti adui yake kisha kummeza akiwahai hivyo sumu ndiyo ilikuwa ikitumika sana katika mapambano yake.

‘’Puuuh…..’’Ni mlio uliosikika baada ya joka lile kuelemewa na mkuki mmoja uliokuwa na sumu kali ulipita karibu kabisa na kinywa chake.‘’Poleni jamani kwa hiyo hamuoni kabisa?’’Aliongea Yule aliyeurusha ule mkuki akimsogelea Yule myoka mkubwa kabisa ambaye akipita sehemu ni kama gari lilikuwa limepita.

‘’Ndiyo lakini si mbaya umasikini kwa heri’’Aliongea mmoja kati ya wawili waliokuwa wamepoteza uwezo wow a kuona akijikuna kalibu kabisa na jicho lake bado kazi kubwa sana kumchuna ngozi yake ya tumbo na kufanikiwa kupita nayo hadi kufika Ukerewe kwa mtaalamu’’Aliongea mwingine huku lafudhi yake ya kihehe ikishindwa kujificha.

‘’Harafu yure ariyerara pale ni nai’’Aliongea Mwita ambaye alikuwa ni kama kiongozi wao.
‘’Sasa we Mkurya unaniuliza mimi wakati sioni si utani huu?’’Alisikika kijana mwingine aliyeonekana ni kabila watani na wakurya ambaye licha ya kupoteza uwezo wake wa kuona furaha yake ya kuukwepa umasikini ilimfanya asijute kabisa kupatwa na tatizo lile.

‘’Ngoja tukamwone aliinuka Mwita akiwaacha wenzake wakiendelea kumchuna Yule nyoka ngozi yake ya tumboni.
Lakini kabla hata ya kumfikia Yule binti mvua kubwa ilianza kunyesha eneo lile walilokuwa na hata walipojaribu kutoka kuna nguvu ya ajabu iliwazuia kufanya hivyo.

‘’Haya maajabu mvua gani ituzunguke sisi pekee?’’Alisikika kijana mwingine akiacha kufanya kazi ya kumchuna Yule nyoka.

ITAENDELEA
Je,walifanikiwa kutoka na ile ngozi?

Kuna uhusiano gani na mama Muuaji na hawa watu?

No comments: