wenyeviti wa ccm wa kata za wilaya ya Ludewa wakiwa katika picha ya pamoja
makatibu waenezi wa ccma kata za Ludewa wakiwa katika picha ya pamoja
Mwenyekiti wa ccm wilaya ya Ludewa Stanley Kolima akisalimiana na Mh.Kawawa katika viwanja vya Bunge
Waziri mkuu Mh.Pinda akiwa na Deo Filikunjombe akiwasalimia wajumbe wa wilaya ya Ludewa katika viwanja vya Bunge
Wajumbe wakiwa katika picha ya pamoja na Mbunge wao Filikunjombe katika viwanja vya bunge
Filikunjombe akiwa na Kapteni Komba
Makatibu wa ccm kata za Ludewa wakiwa katika picha ya pamoja
kapten Komba akiongea na wajumbe
Makamu mwenyekiti wa ccm Taifa Bw.Philipo Mangula akiongea na wajumbe
wajumbe wakiwa bungeni
Filikunjombe akitoka na wajumbe bungeni
waandishi kutoka Ludewa akiwa na Filikunjombe katika viwanja vya bunge
Wabunge wa chama cha mapinduzi(CCM) na
wale wa upinzani wamewataka wananchi wa wilaya ya Ludewa katika mkoa
wa Njombe kubaki njia kuu kwa kuendelea kubaki na Deo Filikunjombe
katika uchakuzi ujao na kuacha tabia iliyozoeleka wilayani hapo ya
kubadirisha wabunge kila kipindi.
Kauli hiyo ilitolewa jana na wabunge
hao katika hoteli ya kimataifa ya St.Gaspar iliyoko mjini Dodoma
ambao walishiriki chakula cha jioni na viongozi 100 wa chama cha
mapinduzi kutoka kata 25 za wilaya ya Ludewa waliosafirishwa na
Mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe kwa lengo la kushiriki
bunge la katiba na kupata mafunzo mbalimbali ya utawala.
Baadhi ya wabunge walioshiriki katika
chakula hicho ni pamoja na Hilda Ngoye mbunge wa viti maalumu mkoa wa
Mbeya ccm,Rita Kabati Iringa viti maalumu ccm,Gaudens Kayombo wa
Mbinga na Kapten John Komba wa Nyasa,mwingine ni Kangi Lugola wa
Mwibala,hao ni baadhi ya wambunge.
Wakiongea kwa Nyakati tofauti Mbunge wa
wilaya ya Nyasa kapten John Komba lisema ni muda mrefu mikoa ya
kusini imekuwa nyuma kwa maendeleo lakini kutokana na kupata wabunge
makini ambao ni wasemaji bungeni na wanauchungu na wapigakura wao
Serikali imesikia kilio chao na tayari maendeleo yameanza kuonekana.
Kapten Komba alisema wilaya ya Ludewa
inasifika kwa kubadirisha wabunge kwa kila kipindi hali ambayo
imesababisha kutokuwa na maendeleo kutokana na viongozi hao kuwa na
mipango mizuri lakini kabla ya kutimiza mipango hiyo hutolewa
madarakani.,
“Nawaomba wanaludewa muache tabia
hiyo ya kuwabadili wabunge kama nguo,mmekuwa nyuma kwa miaka mingi
katika maendeleo lakini hili jembe mlilolipata sasa msilipoteze kwa
kudanganywa na wapenda madaraka ambao hawatawaletea
maendeleo”,alisema John Komba.
Aidha Mh.Hilda Ngoye ambaye ni mzaliwa
wa kijiji cha Nsisi kata ya Lifuma wilayani Ludewa aliwasihi wajumbe
hao kwa kupiga magoti akisema imefika wakati wilaya ya Ludewa
inatakiwa kuwa na mtu mpenda maendeleoa ambaye si mwingine bali ni
Deo Filikunjombe.
Mh.Ngoye alisema ni miaka mingi kata za
mwambao wa ziwa nyasa zimekuwa zikipata shida kubwa ya mawasiliano na
Barabara hali iliyosababisha wananchi wengi hasa akina mama
wajawazito kutembea kwa miguu kwa zaidi ya kilometa 45 kwa kufuata
huduma za Afya lakini kwa sasa mambo yameanza kubadirika na
wanaludewa kufaidi matunda ya uhuru.
Alitolea mfano barabara ya Ludewa
Lupingu ambayo ilikuwa tatizo na kusababisha ajali mbaya kutokana na
ukubwa wa safu ya milima Living stone lakini kipindi ambacho
Filikunjombe ameingia madarakani ameweza kuishawishi Serikali na
barabara hiyo umepata fedha za upanuzi na kuingizwa katika mpango wa
Tanroad.
Mh.Ngoye alisema hiyo ni fahari kubwa
na nikitu cha kujivunia kuwa na mbunge mwenye mawazo mazuri ambaye
anawajali wananchi wake hivyo hakuna sababu ya kuhangaika zaidi ya
kubaki njia kuu na kuepuka michepuko ya kutafuta kiongozi mingine.
Naye Mh.Deo Filikunjombe aliwataka
wajumbe hao kutoka Ludewa wajifunze mazuri wanayoyaona na si
vinginevyo hata hivyo alisema kuwa lengo la kuandika maneno ya baki
njia kuu acha michepuko katika flana alizowagawia wajumbe hao ni
kuwataka kubaki na CCM na kuacha kuhangaika na vyama vya upinzani
tofauti na wengine wanavyotafsiri.
Ziara hiyo ya mafunzo kwa wajumbe
kutoka Ludewa inatarajia kumalizika tarehe 16 juni mwaka huu ambapo
baada ya kutoka Dodoma watasafiri kuelekea jijini Dar es Salaam
kwaajili ya mafunzo ya kukiboresha chama yaani kuwaandaa vijana kuwa
viongozi na wabaki ndani ya ccm na walioko nje warudi ccm jambo
jingine ni pamoja na mafunzo ya maandalizi ya uchaguzi wa serikali za
mitaa.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment