Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

September 17, 2013

WANANCHI AMANI WAGOMA KUPOKEA TAARIFA YA MWAKA MPAKA WASOMEWE KWANZA TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI YA MIAKA MITANO ILIYOPITA.




             Afisa mtendaji wa kijiji cha Amani Bw.Atanas Mwalongo akiwa ofisini kwake

WANANCHI wa kijiji cha Amani Wilayani Ludewa katika Mkoa wa Njombe wamegoma kupokea taarifa ya mapato na matumizi ya mwaka huu na kuitaka serikali ya kijiji hicho kusoma kwanza taarifa ya mapato na matumizi ya miaka mitano iliyopita ili kuondoa hofu na mashaka juu ya tuhuma za ubadhirifu wa fedha na mali zinazowakabili viongozi wa kijiji hicho.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi wa kijiji cha Amani kinachoongoza kwa kuwa na utajiri wa madini ya dhahabu wilayani Ludewa wamesema hawajawahi kusomewa taarifa ya mapato na matumizi zaidi ya miaka mitano hali ambayo imeanza kuwatia hofu na kutokuwa na imani na uongozi wao.

Kwa upande wake Joseph Mlelwa ambaye ni mkazi wa kijiji cha Amani alisema ni miaka zaidi ya mitano Serikali ya kijiji hicho inaendelea kuwahimiza kushiriki katika shughulu za maendeleo huku wakichangishwa michango mbalimbali lakini hawajui fedha zao zinafanyakazi gani na wala hawana taarifa juu thamani ya nguvu wanazoendelea kuchangia.

“”””kijiji hicho kina miradi mingi ya maendeleo ikiwemo machimbo ya madini aina ya dhahabu,ufugaji,vitaru vya kahawa,Power tiller,Trector na miradi ya ujenzi wa shule ya Sekondari lakini wananchi hawajapata kufahamishwa nini kinaendelea na miradi hiyo imezalisha kitu gani kwa muda mrefu sasa bado tuko gizani katika taarifa ya mapato na matumizi ya kijiji chetu.’’’’’’ alisema Mlelwa

Mlelwa akaongeza kuwa kila kukicha wamekuwa wakishuhudia kubadirishwa kwa maafisa watendaji wa kijiji na si kutoa taarifa ya mapato na matumizi ya kijiji kwa wananchi hali ambayo inawakatisha tamaa wananchi kuendelea kufanya kazi za maendeleo hasa katika shule yao ya kata kama ilivyo maeneo mengine.

“’’’’ tunashangazwa na hali inayotokea kijijini hapa tofauti na vijiji vingine wilayani Ludewa na kijiji hiki ndicho chenye machimbo ya Dhahabu lakini hakuna taarifa zozote za mapato na matumizi licha ya kuwa kijiji hiki kina miradi mingi tofauti na vijiji vingine na hakuna kiongozi yeyote anayeona umuhimu wa jambo hili.’’’’” walilalamika baadhi ya wananchi ambao hawakupenda majina yao yaanikwe.

Waliongeza kuwa mikutano ya hadhara ya kijiji hufanyika na baadhi ya taarifa nyingine hutolewa lakini ikifika muda wa kusoma taarifa ya mapato na matumizi viongozi hao hudai muda hautoshi hivyo taarifa hiyo huahirishwa kila mwaka na hofu ya wananchi ni kwamba kuna uwezekano mkubwa wa harufu na kila dalili za ufisadi.

Afisa Mtendaji wa kijiji cha Amani Atanas Mwalongo alikiri kuwepo kwa tatizo hilo na kusema kuwa ni miaka mitano hivi sasa imepita wananchi wahajaweza kusomewa taarifa ya mapato na matumizi na sababu kubwa bado hazija eleweka kutokana na uongozi uliopita kuhamishwa na wengine kuacha kazi.

‘’’’ tangu nihamie katika kijiji cha Amani ni takribani mwaka mmoja na nusu nimeweza kufanya kazi kijijini hapa lakini kila nikitaka kutoa taarifa yangu kwa kipindi nilichokuwepo wananchi hukataa na kutaka zisomwe taarifa za miaka mitano ya nyuma wakati yeye hahusiki na taarifa hizo kutokana na aliyekuwa mtendaji wa kijiji hicho kuhamia kijiji cha Mfarasi.’’’’’ alilalamika Mwalongo

Mwalongo akaongeza kuwa amejaribu kufanya mawasiliano na Afisa mtendaji aliyempokea Oktavian Mtewele aliye hamia kijiji cha Mfarasi bila mafanikio hivyo bado anaendelea kufuatilia taarifa za awali ili kumaliza mgogoro kwa wananchi ambao ni haki yao kufahamishwa mapato na matumizi ya kijiji chao.

Kwa mujibu wa wananchi kijiji hicho kina miradi mingi ya maendeleo na hivi sasa kuna baadhi ya madarasa yanakarabatiwa ili yaweze kufunguliwa na mbio za mwenge wa Uhuru hivyo wananchi wanapaswa kushikamana katika kuhakikisha kazi za maendeleo zinatekelezeka na si kususia.


No comments: