Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

June 06, 2013

WATENDAJI LUDEWA WAKWAMISHA MRADI WA UMEME VIJIJINI



Haya ndio maporomoko ya mto Lupali wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe ambako umeme utazalishwa na shirika la LCBA na kusambazwa zaidi ya vijiji 19
Baadhi ya wajumbe wa shirika hiilo wakiangalia maporomoko ya mto Lupali
 Wajumbe wa LCBA wakiiwa na wataalamu katika upimaji
misitu iliyoko katika mto Lupali
 wajumbe wakiwa na wataalam wa masuala ya Ardhi
      misitu ya mto Lupali

VIONGOZI wa vijiji wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe wametajwa kuwa kikwazo cha uharakishaji wa mradi wa umeme unaotarajiwa kuzalishwa katika maporomoko ya mto Lupali kata ya Mundindi kutokana na viongozi hao kushindwa kukusanya michango kwa wananchi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo katibu wa shirika la Ludewa Capacity Building Association(LCBA) Bw.Joseph Kayombo alisema zoezi la upembuzi yakinifu katika vijiji zaidi ya kumi na tisa ulitakiwa kuanza june mosi mwaka huu lakini imeshindikana kutokana na wenyeviti na watendaji katika vijiji husika kushindwa kukusanya asilimia 20  ya fedha kutoka kwa wananchi.

’’’’ mamlaka ya usambazaji umeme vijijini Rular Enegy Agecy (REA) ilishatoa mwongozo juu ya miradi hiyo ambapo kila kijiji kinatakiwa kuchangia gharama ya nguvukazi na fedha 2% ili kukamilisha mradi huo lakini mpaka sasa baadhi ya viongozi wa vijiji wamekuwa kikwazo kwa kushindwa kufanya kazi hiyo.’’’’’ Alilalamika Kayombo

Kayombo aliongeza kuwa lengo la REA ni kumtaka mwananchi achangie japo kidogo ili aweze kujiona naye ni sehemu ya mradi huo katika umiliki lakini mpaka sasa mamlaka hiyo imeshatoa fedha za awali kinachosubiriwa ni michango ya wananchi ili kazi ianze.

Alisema shirika lake ndilo shirika pekee lililopewa dhamana ya kuusimamia mradi huo na tayari liko katika hatua nzuri lakini kinachosikitisha ni baadhi ya watendaji na wenyeviti wa vijiji kushindwa kukamilisha makubaliano ya michango ili kazi ianze.

“tulikubaliana mwisho wa kuileta michango yao ni Mey 30 mwaka huu ili Juni 1 kazi ianze lakini mpaka sasa viongozi hao wamekuwa wakitoa ahadi bila utekelezaji hali ambayo inatuchelewesha kuanza kazi za mradi huo wa umeme ambao utaleta manufaa makubwa kwa wananchi na Taifa”,alisema Bw.Kayombo.

Bw.Kayombo alisema umeme huo unakadiliwa kutoa megawalt 30 ambazo zitavinufaisha zaidi ya vijiji 19 kwa gharama nafuu kutokana na shirika hilo kujihusisha na utoaji misaada na elimu katika maeneo mbalimbali ndani ya wilaya ya Ludewa.

Alivitaja vijiji vitakavyonufaika na huduma hiyo katika kata ya Mundindi kijiji cha Mundindi,Amani na Njelela,kata ya Ibumi ni kjiji cha Ibumi na  kata ya Madilu ni kijiji cha Madilu,Ilininda,Ilawa,Mfalasi na Manga kata ya Madope kijiji cha Madope,Luvuyo na Mangalanyene.

Vijiji vingine ni Mkongobaki,Lipangala,Ugela,Shaurimoyo na Mdilidili,Mbwila na Luana hata hivyo alisema umeme huo utakuwa na nguvu kubwa hivyo unaweza kusambaa katika vijiji vingi zaidi itakavyowezekana kutokana na wafadhiri wa mradi huo watakavyopendekeza.

Aidha mjumbe wa shirika la LCBA Bw.Lazaro Mwinuka alifafanua kuwa shirika hilo unakadiliwakutumia  kiasi cha shilingi 40 Bilion kutoka Bank ya Dunia kupitia REA ambazo zitafanya kazi zote mpaka mradi huo utakapo kamilika.

Bw.Mwinuka alisema mchakato wa mradi huo umeshaanza lakini unatarajia kumamilika ifikapo mwaka 2014 kutokana na ukubwa wa mradi hivyo wananchi wa vijiji tajwa wanatakiwa kuanza maandalizi katika nyumba zao ili waweze kunufaika na mradi huo.

Alisema kama watendaji wa vijiji watakamilisha michango yao haraka basi mradi huo unakamilika mapema ili kuwapa fulsa wananchi kuanza kunufaika kabla ya machimbo ya mchuchuma na Liganga
Mwisho.

No comments: