Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

June 17, 2013

VIONGOZI WA LUDEWA KIJIJINI WALAUMIWA KWA KUSHINDWA KUSOMA MAPATO NA MATUMIZI YA KIJIJI.



 
WANANCHI wa kijiji cha Ludewa (K) wilaya ya Ludewa katika mkoa wa Njombe wametishia kugoma kutoa michango pamoja kutojihusisha na shughuli za maendeleo kijijini hapo kama  uongozi utashindwa kutoa taarifa ya mapato na matumizi haraka.

Hatua hiyo imekuja kutokana na uongozi kushindwa kuitisha mkutano wa hadhara kijijini hapo kwa ajili ya kutoa taarifa ya mapato na matumizi na kupelekea wananchi kukosa imani na uongozi huo akiwemo mwenyekiti wa serikali ya kijiji Dizbody Nkinga na afisa mtendaji wake Oraph Kiowi.

Wakizungumza jana kwa nyakati tofauti wananchi hao walisema kwa mara ya mwisho mkutano kwa ajili ya  kusoma  taarifa ya mapato na matumizi ya kijiji chao ilitolewa julai 2 mwaka jana ambapo hata hivyo taarifa haikuwa ya kuridhisha ilikuwa na mapungufu mengi.

‘’’’ sisi wananchi tunaendelea kutozwa michango mbalimbali kila kukicha kijijini hapa lakini hatuelewi viongozi wetu wamekusanya mapato kiasi gani na matumizi yaliyofanyika hali ambayo inatukatisha tamaa kabisa ni bora tuache kuchangia shughuli za maendeleo kutokana na kutokuwa na uwazi katika makusanyo na matumizi.’’’’ alisema mkazi wa kijiji hicho ambaye hakupenda jina lake liandikwe

Aidha afisa mtendaji wa kijiji hicho Bw.Oraph Kiowi alikili kuwa ofisi yake haijaweza kuwasomea wananchi taarifa za mapato na matumizi kwa muda mrefu hivyo wananchi hao wanahaki ya kuulalamikia uongozi wa kijiji hicho.

Kiowi alisema tatizo la kutosoma taarifa hizo ni kutokana na ushirikiano mdogo anaoupata kutoka kwa wenyeviti wa mitaa ambao ni wajumbe wa halmashauri ya kijiji kwa kutohudhuria katika vikao vya ndani kila anapoitisha vikao hivyo.

Nae mwenyekiti wa kijiji hicho Disbody Nkinga alisema kumekuwa na kutoelewana kati ya wenyeviti wa mitaa na afisa mtendaji wa kijiji hivyo kusababisha kukwamisha shughuli za maendeleo kutokana na wenyeviti hao kushindwa kufanya kazi zao.

Nkinga alisema mwaka 2012 alimuandikia barua na kumjulisha mtendaji wa kata ya Ludewa kuhusiana na tatizo la wenyeviti hao wamitaa na wajumbe wa halmshauri ya kijiji kutohudhuria vikao vya ndani ili kuweza kuwasomea wananchi taarifa za mapato na matumizi na kushindwa kukusanya michango ya maendeleo.

Maamuzi yaliyofanyika na ofisi ya kata ilikuwa ni kuwachukulia hatua za kisheria ambapo majina yao yalifikishwa mahakamani na wakatakiwa kwenda kijibia mahakamani lakini wenyeviti hao walitoroka na kwenda kusiko julikana,na mpaka sasa wengine wanaendelea na kazi lakini bado tabia yao ya kutofuatilia michango inaendelea.

Bw.Nkinga aliwataka wananchi kuwa waangalifu wanapochagua viongozi wa mitaa richa ya wananchi hao kuushutumu uongozi mzima wa kijiji kuwa unashiriki katika kudidimiza maendeleo ya kijiji hicho kwa kutafuna michango ya wananchi.
Mwisho.

No comments: