Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

June 04, 2013

BANK YA NMB TAWI LA LUDEWA YAWATAKA WATEJA KUWA NA SIRI YA TAARIFA ZAO.





Bank ya NMB tawi la wilaya ya Ludewa katika mkoa wa Njombe imewataka wateja wa benk wilayani humo kuwa na siri ya taarifa zao ili kuepusha wizi wa fedha unaoweza kuwakumba wateja hao.

Akiongea na waandishi wa habari jana meneja wa bank ya NMB lawi la Ludewa Bw.Maulid Abdalah Mwingira alisema kumekuwa na wateja ambao hawana siri juu ya taarifa zao za kibenk hali ambayo inasababisha wateja hao kuibiwa fedha zao na kuilaumu bank wakati kosa liko kwa wateja hao.

Alisema baadhi ya wateja wamekuwa wakiwaamini sana watoto na jamaa na marafiki zao na kuwapatia namba za siri za account zao na baadae kuibiwa fedha bila kujitambua na kupelekea kuilaumu bank bila msingi wowote.

“napenda kuweleza wateja wetu kuwa wasipende kutoa taarifa zao za kibenk kwa kila mtu kwani wanaweza kuibiwa fedha zao na watu wanaowaamini,na watambue kuwa kupitia mitandao ya simu mtu anaweza kuhamisha fedha kutokana na wewe kumpa taarifa zao za kibenk”,alisema Bw.Mwingira.

Bw.Mwingira alisema Bank hiyo ina wateja wengi sana nchini na kama kila mteja atakuwa na tabia ya kutunza taarifa zake vizuri basi hakuna mtu mwingine atakayeweza kuiba fedha katika account ya mwingine lakini kama mteja mwenyewe hatakuwa na siri katika taarifa zake basi ataruhusu kuingiliwa.

Aidha aliwataka wanaoibiwa kwa uzembe wao wenyewe wasiwe na kauli ya kuichafua bank hiyo kwani wafanyakazi wa bank ya NMB Tanzania ni waadirifu na wako makini na kazi wanazozifanya na si vinginevyo

Kuhusiana na Mitandao ya simu kuathiri huduma za kibenk Bw.Mwingira alisema hakuna athari yoyote ya mitandao hiyo katika shughuri za kibenk kutokana na mahusiano mazuri ya mitandao hiyo na Bank.

Alisema kupitia mitandao ya simu wateja wa bank wanaweza kuweka na kutoa fedha bila ya kufika bank hali ambayo imewarahisishia wafanyakazi wa bank kutokuwa na mzigo mkubwa na kuweza kukusanya marejesho ya mikopo kwa kutumia mitandao hiyo.

Bw.Mwingira alisema kila kitu kina faida na hasara ndivyo ilivyo mitandao ya simu katika huduma za kibenk kwani kuna watu ambao pia hutumia mitandao hiyo katika wizi wa fedha nchini kwa baadhi ya bank.

Hali ambayo inawafanya wafanyakazi wa bank kuwa makini na kazi yao na katika kufuatilia account zote ili kubaini kama kuna wizi unaoweza kujitokeza kwa kutumia mitandao hiyo na waliobainika kutumia vibaya mitandao ya simu wameshachukuliwa hatua za kisheria ili kukomesha wimbi la wizi wa mitandao.

Bw.Mwingira aliwataka wateja kuwa waangarifu na taarifa zao pia kuuliza kwa wafanyakazi wa bank hiyo pale wanapoona kunautata ama hawajaelewa na si kulaumu kwa vitu wasivyovifahamu,ili kupata ufumbuzi mapema iwezekanavyo.

Mwisho.

No comments: