Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

May 22, 2013

WAZAZI WILAYANI LUDEWA WATAKIWA KUFUATILIA MAENDELEO YA WATOTO WAO WAWAPO SHULENI


 Mwalimu Paulo Matunduru ambaye ni Mwalimu mkuu wa Shule ya Sekondari Ludewa akiwa katika bweni la wavulana
Mazingira ya Shule ya Sekondari Ludewa ambayo ni shule ya wazazi inayomilikiwa na Chama Cha Mapinduzi(CCM)
Baadhi ya majengo ya shule ya Sekondari ya Ludewa
    Dada mkuu wa shule hiyoCraudia Nkwera na Kaka mkuu Joel Kayombo

Wazazi wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe wametakiwa kutoa ushirikiano kwa walimu wa shule za Sekondari na Msingi ili kuleta ufanisi wa elimu kwani kushuka kwa elimu kunatokana na wazazi hao kutofuatilia maendeleo ya watoto wao.

Hayo yalisemwa na mwalimu mkuu Paulo Matunduru wa shule ya sekondari Ludewa shule ya wazazi ambayo inamilikiwa na chama cha mapinduzi wakati akiongea na waandishi wa habari walipokwenda kumtembelea katika shule yake.

Mwalimu Matunduru alisema,wazazi wengi hawafuatilii maendeleo ya watoto wao pindi watokapo shule hali ambayo inawafanya wanafunzi walio wengi kujisahau na kuwa wazembe madarasi kielimu.

Alisema kama walimu na wazazi watashirikiana kikamilifu katika kufuatilia maendeleo ya wanafunzi basi tatizo la kufeli katika mitihani litapungua kwa kiasi kikubwa nchini na malalamiko ya wadau wa elimu hayatakuwepo.

“kama wazazi watashirikiana na walimu katika kufuatilia maendeleo ya wanafunzi kuanzia shule za msingi na zile za sekondari kwa kukagua daftari na mitiahani wanaporudi majumbani hali ya elimu nchini itakua na hata kiwango cha ufaulu katika mitiahani kitaongezeka”,alisema Mwalimu Matunduru.

Alisema imefikia wakati baadhi ya wazazi wamesahau wajibu zao kwa kuwatelekeza watoto mashuleni na kutofuatilia maendeleo yao hali ambayo inasababisha wanafunzi wengi kufanya vibaya kutokana na kukosa ufuatiliaji.

Aidha alizitaja changamoto zinazo ikumba shule hiyo ikiwa ni pamoja na ukosefu wa bwalo la chakula kwani mpaka sasa uongozi wa shule umelazimika kutenga chumba kimoja cha darasa kutumika kwaajili ya chakula.

Alisema shule hiyo inampango wa kuanzisha masomo ya kidato cha tano na cha sita lakini bado majengo yake yanahiotaji ukarabati mkubwa ikiwemo ujenzi wa bwalo la chakula ili kukidhi mahitaji ya wanafunzi.

Changamoto nyingine inayoikabili shule hiyo ni pamoja na ubovu wa barabara ya kuingia shuleni hapo kwa baadhi ya gari zinashindwa kuingia kutokana na barabara ya awali kuharibika vibaya na mvua.

Mwalimu Matunduru aliwaomba wahusika wakuu wa shule hiyo kusaidia kukabili changamoto hizo kwani ni shule kongwe wilayani hapa hivyo haipaswi kusahaulika kiasi hicho ikizingatiwa im ezalisha wasomi wengi wanaofanya kazi katika kada mbalimbali Serikalini na binafsi.

Mwisho.

No comments: