Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

May 29, 2013

KINANA AWAFUNDA WANANCHI WA WILAYA YA LUDEWA MKOANI NJOMBE.





Kushoto katibu mkuu wa CCM Bw.Kinana akiwa na mbunge wa jimbo la Ludewa Bw.Deo Filikunjombe



katibu wa itikadi na uenezi  wa CCM Taifa  Nape Nnauye akisalimiana na wananchi wa wilaya ya Ludewa

Katibu mkuu wa CCM Taifa Bw.Kinana akisalimiana na Baba mzazi wa Mbunge wa jimbo la Ludewa Mzee Filikunjombe
 Kinana akiongea na wananchi wa kata ya Ludewa mjini
Wananchi wakimsikiliza mbunge wao Deo Filikunjombe hayupo pichani
 Wananchi wakifuatilia mkutano wa hadhara

Katibu mkuu wa chama cha mapinduzi Taifa Bw.Abdulrahman Kinana jana aliwahakikishia wananchi wa wilaya ya Ludewa katika Mkoa wa Njombe kuwa viwanda vya uzalishaji wa chuma na makaa yamawe vitajengwa wilayani humo na si kwingineko.

Kauli hiyo ya Kinana imekuja baada ya kuvuma tetesi kuwa viwanda hivyo kunauwezekano mkubwa wa kujengwa Bagamoyo hivyo wananchi wa wilaya ya Ludewa walikuwa na shauku ya kujua ujemzi wa viwanda hivyo.

Alisema kutokana na ukubwa wa miradi hiyo miwili ambayo inatarajia kuanza miaka ya 2015 na 2016 na kubadiri taswira nzima ya wilaya ya Ludewa haitaweza kujengwa eneo jingine zaizi ya wilaya hiyo na kusambaza umeme huo nchi nzima.

Bw. Kinana aliwataka wananchi wa wilaya hiyo kuwa makini na watu wanaoeneza habari za uwongo ambazo zinalengo la kujenga chuki miongoni mwa jamii na viongozi kwani kinachotakiwa zaidi ni kuisikiliza Serikali kupitia kwa Mbunge wa jimbo hilo.

“Tumekuwa tukifanya kazi vizuri na Mbunge wenu Filikunjombe hivyo kinachotakiwa kumsikiliza na kumuamini kwani chochote anachowaeleza kinatoka Serikalini na si vinginevyo hata hao wanowadanganya kuhusiana na ujenzi wa viwanda wakataeni”,alisema Bw.Kinana.

Alisema Serikali ya CCM inafurahishwa na utendaji wa Mh.Deo Filikunjombe kwani ni mfano kwa wabunge wengine wa chama hicho kutokana na kujiamini katika kutetea wananchi wake awapo Bungeni.

Katika hatua nyingine Wananchi wa  jimbo  hilo walionyesha  kumbana  kiongozi huyo kwa  kuhoji  sababu ya wabunge  wa CCM bungeni  kufanya kazi ya kukipongeza chama  chao  huku  wengi  wao  wakiwa kimya (mabubu) katika  kuchangia na  wale  wanaochangia kama mbunge  wao Filikunjombe  wamekuwa  waklichukiwa kuwa ni  wapinzani ndani ya CCM . 

Hivyo  wananchi hao  kumweleza katibu mkuu  huyo aliyeongozana na katibu wa itikadi na uenezi  wa CCM Taifa  Nape Nnauye  kuwa wao  wataendelea  kumuunga mkono mbunge Filikunjombe kwa  vipindi  vingine  tena  vitatu vya miaka 15  hadi mbunge mwenyewe  atakapoamua  kuacha  kugombea na iwapo watafanya mchezo  basi wao watamfuata  mbunge  huyo kokote atakakokuwa.

" Mheshimiwa  tunaomba  leo chama kitueleze  hivi  kwanini wabunge wa CCM wamekuwa  si msaada kwa wapiga  kura  wao muda  wote  wamekuwa  kimya  bungeni na  wale  wanaochangia  wanachangia kupongeza  chama,  tunaomba  kukueleza  kuwa sisi  tupo na mbunge  wetu  na hata  wana  CCM wanaojipitisha jimbo la Ludewa  wakiamini  sisi tutayumba  uwaeleze  kuwa CCM hatudanganyiki  "alihoji mwananchi aliyejulikana kwa jina la Optatus Kalungu.

Akizungumza jana  na  wananchi  wa  wilaya ya  Ludewa ambao  walikusanyika kwa wingi katika mkutano  wa hadhara  kwa lengo la kutaka  kusikia kauli ya CCM juu ya uamuzi  utakaochukuliwa kwa mbunge   wao kutokana na kuwepo kwa kauli  za chini kwa chini katika jimbo  hilo kuwa ziara ya Kinana jimboni  humo ni kutaka  kumshughulikia mbunge  huyo.

Hata  hivyo Kinana aliwataka  wananchi wanaounga mkono uamuzi  wa kuendelea  kumwongezea muda wa vipindi  vitatu Filikunjombe  kunyosha  mikono  juu na baada ya  wananchi  wote  kunyosha  mikono yao  juu alisema pia kwa upande  wake anaungana na wao na kuwa chama hakitafanya makosa kwa  kuwasaliti  kuwapa mtu mwingine katika  uchaguzi ujao wa mwaka 2015 . 

"Hata  mimi katibu  mkuu naungana na uamuzi wenu wa  kumwongeza muda Filikunjombe na  napenda  kuwahakikishia  kuwa CCM haitafanya makosa  itaendelea  kuwaachia Filikunjombe kama mlivyomchagua wenyewe  labda ashindwe  yeye " alisema Kinana.

 Kwa  upande  wake Filikunjombe alisema mbali ya  kuanza mradi mkubwa wa lami katika wilaya  hiyo wa kuanzani Itoni Njombe hadi Manda ila bado kuna mradi  wa maji wenye thamani ya Tsh bilioni 1.5 ambao utaondoa adha ya maji katika  mji  wa Ludewa ambayo ndio kero kubwa kwa wananchi wake. 

Filikunjombe  alisema  katika mji wa Ludewa tayari Serikali imetenga fedha za kutengeneza barabara za mitaa kwa kiwango cha lami kilometa kumi na ujenzi huo unaanza mara moja hivi punde hivyo wananchi wanatakiwa kutoa ushirikiano kwa kampuni iliyopewa tanda hiyo.

Alisema kutokana na kuendelea  kuutamani ubunge  wake ataendelea  kuwatumikia vema  wananchi na kamwe siku  zote hatarudi nyuma bungeni katika  kuwapigania  wananchi hao

Mwisho.

No comments: