Kinana akisaini kitabu cha wageni Uwanja wa Ndege wa Iringa baada ya kuwasili uwanjani hapo asubuhi jana. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa, Joyce Msavatavangu
Nape
akisaini kitabu cha wageni
Katibu
Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape
Nnauye wakisalimia baadhi ya viongozi, baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa
Iringa asubuhi jana, kwa ajili ya kuanza ziara ya siku saba, mkoani Njombe.
Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa, Joyce Msambatavangu.
Katibu
Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwa na viongozi wa mkoa wa Iringa.
Nyuma ni Nape Nape naye akiwa na wenyeji.
Katibu Mkuu wa CCM Taifa Mhe.Kinana
afanya mazungumzo na Wakazi wa Iringa Mapema jana kabla ya kuanza safari ya Siku
sita Mkoani Njombe kuanzia leo may 27
Katika hatua Nyingine Katibu Kinana na
Katibu Mwenezi wa CCM Taifa Nape Mnauye watafanya kazi ya kuzindua tawi la
Chama katika Eneo la Mizani MAKAMBAKO Mkoani Njombe pamoja na Kuzungukia Wilaya
zote za Mkoa wa Njombe.
Aidha Katibu Kinana atawasili Wilayani
Makete May 30 mwaka Huu na Julai Mosi mwaka Huu atakuwa Wilaya ya
Wanging'ombe.
Majira ya Alasiri Kinana atawasili
Mkoani Njombe na Msafara wake tayari kwa Ziara ya Siku sita Mkoani Njombe.
Kesho May 28 mwaka huu katibu
huyo pamoja na Msafara wake atakuwa Wilayani Ludewa na May 29 atakuwa Wilayani
Njombe kabla ya Kuwasili Wilayani Makete may 3o mwaka Huu.
Kwa Mujibu wa Taarifa za Ndani ya Chama
cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Njombe Kupitia katibu wake Mkoa bwana Hosea
Mpagike,Kinana atafanya ziara na Kuondoka Juni Mosi Wilayani Wanging'ombe
Mkoani Njombe.
Na Gabriel Kilamlya,Njombe.
No comments:
Post a Comment