Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

October 06, 2012

UCHELEWESHAJI FEDHA TOKA HAZINA KIKWAZO CHA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI


Na Nickson Mahundi,Njombe.

Ucheleweshaji wa fedha za miradi ya maendeleo kutoka Serikali kuu imekuwa kikwazo kikubwa cha utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri za Mkoa wa Njombe.

Tatizo hilo limezikumba Halmashauri nyingi nchini kutokana na fedha hizo kutoletwa kwa wakati hivyo kuzifanya Halmashauri kupata hati chafu wanapopita wakaguzi na kuona fedha nyingi zikiwa hazijatumika.

Hayo yalisema jana katika kikao cha ushauri cha Mkoa wa Njombe(RCC) ambacho ni kikao cha kwanza tokea mkoa huu uanzishwe na baadhi ya wakurugenzi wa Halmashauri wa wilaya mbalimbali mkoani hapa.

Akilitolea ufafanuzi suala hilo Mkuu wa mkoa wa Njombe Kapten Assery Msangi alisema ofisi yake inalitambua hilo na kusisitiza ataendelea kuiomba Serikali kuu kuzileta fedha hizo mapema ili ziweze kutomika kwa muda unaofaa.

Kapten.Msangi alisema ifike wakati Halmashauri ziibue na kubuni miradi itakayosaidia katika makusanyo ya mapato ya ndani ili kukamilisha miradi kwa wakati kuliko kutegemea mapato ya nje.

“tumekuwa na utamaduni wa kutegemea mapato ya nje zaidi lakini ninachotaka mkoa wangu uwe wa mfano katika ukusanyaji wa mapato ya ndani kwani kumekuwa na udhaifu mkubwa katika ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri mbalimbali”,alisema Kapten Msangi.

Kuhusu mgawanyo wa mali za mkoa mama wa Iringa wajumbe walilalamikia kutogawiwa chochote kutokana na ujenzi wa mkoa huo ulifanyika na mkoa wa Njombe pia.

Lakini cha kushangaza Mkoa wa Iringa haukufanya mgao wowote kwa mkoa wa Njombe hali hiyo iliwasikitisha wajumbe na kuahidi kulifuatilia suala hilo kwa kina ili kupata ufumbuzi.

Aidha kikao hicho kilipitisha kupandishwa hadhi kwa Hospitari ya Kibena kuwa ya Mkoa ili kusogeza huiduma za afya zenye hadhi ya mkoa na kuvutia waewkezaji katika mkoa mpya wa Njombe.

Hatua hiyo ilifuatia baada ya kuonekana ukosefu wa fedha za ujenzi wa hospitari ya mkoa ambapo eneo la ujenzi wa hospitari hiyo lilishaandaliwa kinachosubiriwa ni ramani na fedha za ujenzi wa Hospitairi hiyo.

Kwa upande wa kilimo Mkoa wa Njombe ulionekana kuwa na wafanyabiashara wengi wanaotoka nchi ya Kenya na kwenda moja kwa moja kwa wakulima ambao huwarubuni kwa kununua viazi kwa rumbesa.
Hali hiyo iliwafanya wajumbe kuhoji ujenzi wa soko la kimataifa katika mji wa Mkambako ambalo limeongelewa kwa miaka mingi bila ya utekelezaji hali hiyo ndiyo inayosababisha biahsra ya lumbesa.

Akizungumza kuhusiana na soko hilo Mbunge wa Makambako Bw.Deo Sanga(Jaa people) alisema ni muda sasa wananchi wa Makambako alikataliwa kuyaendeleza maeneo ya soko hilo lakini hakuna utekelezaji.

Kapten Masangi aliahidi kulifuatilia hiyo kwa uwepo wa soko la kimataifa katika mkoa wa Njombe ni ukombozi mkubwa kwa wakulima kutokana na kukoa huo kuwa na kilimo cha mazao mbalimbali.

Changamoto kubwa ya mkoa huo ilionekana ni upungufu wa wafanyakazi katika sekta mbalimbali,uchomaji misitu,uhaba wa maji safi na salama na ukosefu wa soko la uhakika la mazao kwa wakulima.

Hata hivyo kukao hicho kiliazimia kuandaa ufunguzi rasmi wa mkoa huo ili kuwapa fulsa wadau mbalimbali kutambuana na kuwakaribisha wawekezaji katika masuala ya kilimo ikiwemo ujenzi wa viwanda vya kusindika mazao.

MWISHO.

No comments: