Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

September 21, 2012

MAAFISA UGAVI NCHINI WATAKIWA KUTOA TAARIFA SAHIHI


Na Nickson Mahundi,Njombe

Maafisa Ugani nchini wametakiwa kutoa taarifa sahii Serikalini kuhusiana na maendeleo ya sekta ya Kilimo na mifugo kuanzia ngazi ya Vijiji hadi kata ili kuiwezesha Serikali kupanga pajeti inayo stahili katika wizara hiyo.

Hayo yalisemwa jana wilayani Ludewa na Kaimu mkurugenzi msaidizi wa wizara ya Kilimo na Mifugo katika kitengo cha ufuatiliaji na tathmini Bw.John Maige wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kuhusu matumizi ya fomu za kukusanyia taarifa za maendeleo ya kilimo na mifugo kwa maafisa ugani wa vijiji na kata.

Bw.Maige alisema mafunzo hayo yanafanyika katika mikoa sita ya nyanda za juu kusini ili kuwapa uwezo wagani kutunza kumbukumbu na kukusanya taarifa katika mfumo mpya unaofadhiriwa na ASDPM &ETWG ili kupata takwimu sahii toka kwa wakulima na wafugaji.

Alisema mradi huo umegawa pikipiki mbili kila wilaya na moja kwa Hlmashauri za miji pia computer ili kuwezesha mchakato wa utunzaji kumbukumbu,ufuatiliaji na tathmini kufanyika kwa urahisi kuanzia ngazi ya chini na kuendelea.

“Tumeamua kutumia mfumo mpya kutokana na ule wa awali kushindwa kukusanya taarifa kwa usahii hivyo tumegawa vitendea kazi ili kurahisisha kazi hiyo ili tuweze kwenda sawa na mabadiliko ya sera ya kilimo kwanza”,alisema Bw.Maige.

Awali mgeni rasmi akifungua mafunzo hayo ambaye ni kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa Mhandisi.Baraka Mkuya alisema wagani wanapaswa kuwezeshwa kwa kiasi kikubwa ili kuwafikia walengwa katika maeneo ya jiji.

Mhandisi.Mkuya aliwataka wagani waliohudhuria mafunzo hayo kuifanyia kazi elimu waliyoipata kwa kufanya hivyo watakuwa wametimiza adhma ya Serikali katika ukusanyaji wa taarifa za kilimo na mifugo.

Aidha Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU)wilaya ya LudewaBw.Edings Mwakambonja aliwataka maafisa ugani hao kufanya kazi kwa uadirifu kwani kumekuwa na malalamiko ya hapa na pale katika utendaji wao wakiwa vijijin.

Bw.Mwakambonja alisema wananchi wamekuwa wakiilalamikia sekta hiyo kuhusika na kuchukua fedha kama kuchangia huduma pindi wanapohitaji huduma ya matibabu ya mifugo au ushauri katika kilimo hasa maeneo ya mbali na ofisi zao.

Alisema kama afisa ugani anapaswa kuwa mstari wa mbele katika kupinga na kuikataa rushwa anapokuwa katika majukumu yake hivyo wakiona kama kunadalili ya mfanyakazi mwenzao kuchukua rushwa nivema wakatao taarifa mapema ili kuondoa sifa mbaya.

Bw.Maige aliwataka maafisa ugani hao kufanya kazi katika mazingira yoyote kwani ni wachache nchini hivyo wanawakati mgumu kufika kila kijiji kutokana na kutokuwa na vitendea kazi vya kutosha
Mwisho.

No comments: