Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

August 16, 2018

DC LUDEWA AIPONGEZA MITANDAO YAKIJAMII KUCHANGIA MAENDELEO

 Mkuu wa wilaya ya Ludewa Mh.Andrea Tsere akiongea na wanafunzi wa shule ya Sekondari Chief Kidulile ambao waliunguliwa na vifaa vyao katika Bweni.


Mkuu wa wilaya ya Ludewa Mh.Andrea Tsere ameipongeaza mitandao ya kijamii wilayani hapa kutokana na mitandao hiyo kuchangia kiasi kikubwa katika mendeleo ya wilaya katika maafa pia elimu.


Pongezi hizo zimekuja baada ya kikundi cha mtandao kwa njia ya whatsup kijulikanacho kwa jina la group la wilaya ya Ludewa kuandaa mpango wa wanafunzi wa vyuo vikuu wanaotokea wilaya ya Ludewa  kujitolea kufundisha shule za sekondari msimu wa likizo.

Mpango huo unakwenda sambamba na uchangishaji wa fedha katika group la wilaya ya Ludewa,fedha ambazo zitatumika kujikimu kwa wanavyuo ambao wataonesha nia ya kwenda kuinua kiwango cha ufaulu katika shule za Sekondari ndani ya wilaya ya Ludewa.

Mh.Tsere alisema kuwa mpango huo ni wakuigwa kwani mitandao mingi ya kijamii imekuwa ikitumika katika siasa na mambo mengine ya hovyo badala ya kujikita katika kuleta maendeleo kwa wananchi kama inavyofanywa na group la wilaya ya Ludewa.

“niwapongeze kwa juhudi za group hili la wilaya ya Ludewa kwa kuandaa mpango wa maendeleo na kuchangishana fedha ili kuwapatia posho wale watakao jitolea kwani si mara ya kwanza katika group hili kuchangia maendeleo,wamesha saidia ununuzi wa kitanda cha wagonjwa hospitari ya wilaya pia walichangia wakati bweni la shule ya sekondari chief Kidulile lilipoungua hivyo ni mfano wa kuigwa”,alisema Mh.Tsere.

Aidha Mh.Tsere aliwataka wananchi wilayani Ludewa kutoa ushirikiano kwa walimu wanaokuja kujitolea kwani hawalipwi na Serikali hivyo kila mwananchi anawajibu wa kuwalinda kwani wilaya ya Ludewa inaupungufu mkubwa wa walimu wa masomo ya Sayansi hivyo ni fulsa pekee kuwatumia walimu hawa wakujitole ili kukuza kiwango cha ufaulu.

Akitoa ufafanuzi wa mgawanyo wa walimu hao katika shule za Sekondari afisa elimu wa wilaya ya Ludewa shule za Sekondari Mwalimu Matenus Ndumbalo alisema kuwa tayari amewasiliana na walimu wakuu wa shule za Sekondari zote wilayani hapa ili kuwapokea walimu hao.

Mwalimu Ndumbalo alisema kuwa ni kweli wilaya ya Ludewa kunaupungufu mkubwa wa walimu wa masomo ya Sayansi hivyo ni fulsa pekee katika mpango huu wa walimu wa kujitolea ili kuongeza ufanisi katika elimu kwani mpango huu ungeanza muda mrefu ni dhahiri wilaya ya Ludewa ingepiga hatua kielimu.

Mwalimu Ndumbalo aliwataka wanagroup la wilaya ya Ludewa muufanya mpango huo kuwa endelevu kila mwaka ili ufaulu hasa katika masomo ya Sayansi kuongezeka na kushindanda na wilaya nyingine nchini.

Mwisho.


No comments: