Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

August 31, 2017

NICOPOLIS ACADEMY KWA KUSHIRIKIANA NA LUDEWA EDUCATION CENTRE WATOA MSAADA WA CHAKULA SHULE ZA MSINGI KATA YA LUDEWA.

  Mkurugenzi wa Nicopolis Augustino Mwinuka akikabidhi mchele
 Mkurugenzi wa Nicopolis Augustino Mwinuka akikabidhi mchele


 Mratibu elimu kata ya Ludewa Mwalimu Lenis Mtitu
 Makamu Mwalimu mkuu shule ya msingi Kimbila Imani Mtweve akiongea na wageni kutoka Nicopolis Academy na Ludewa education Centre
 Baadhi ya majengo ya shule ya msingi Ludewa Mjini
  Mkurugenzi wa Nicopolis Academy Mwalimu Augustino Mwinuka akiongea na wanafunzi wa darasa la saba shule ya msingi Ludewa mjini mara baada ya kukabidhi msaada wa mchele

 Mkurugenzi wa Nicopolis Academy Mwalimu Augustino Mwinuka akiongea na wanafunzi wa darasa la saba shule ya msingi Ludewa mjini mara baada ya kukabidhi msaada wa mchele
Kulia  Mwalimu mkuu wa shule ya Msingi Ludewa mjini Mathew Haule akiwa na wageni wa Nicopolis pamoja na Ludewa Education
 Wanafunzi wa darasa la saba wa shule ya msingi Kimbila wilayani Ludewa wakiwa darasani




Kituo cha watoto waishio katika mazingira hatarishi wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe cha Nicopolis academy pre &primary English medium school kwa kushirikiana na Ludewa education Centre wametoa msaada wa chakula kwa wanafunzi wa darasa la saba katika kata ya Ludewa.


Akikabidhi msaada huo kwa walimu wa shule za msingi kata ya Ludewa mkurugenzi wa Nicopolis Academy Mwalimu Augustino Mwinuka alisema kuwa wamefikia hatua ya kutoa msaada huo wa mchele kwa wanafunzi wa darasa la saba ili kuwawezesha kupata chakula siku mbili za mtihani wa Taifa unaotarajia kufanyika hivi karibuni.


Mwalimu Mwinuka alisema kuwa baadhi ya wazazi na jamii kwa ujumla wamekuwa wakutoa lawama kwa walimu pale matokeo yanapokuwa mabaya bila kujali wao kama jamii wanamchango gani kwa wanafunzi hasa kipindi cha mitihani ya mwisho,hivyo kabla ya kulaumu ni vyema kutambua wajibu wa jamii kwanza ndipo zitolewe lawama kwa walimu.


Alisema kuwa watoto wanapopata chakula cha aina moja kipindi cha mitihani inaweza kusaidia katika ufaulu kwani ikiwa kila mmoja atapata chakula kutoka nyumbani kwake wengine hawana uwezo mzuri wanakotoka hivyo hujikuta wanyonge wanapoona wenzao wanaletewa vyakula vya aina Fulani na wazazi wao na hali hiyo hupelekea kufanya vibaya katika chumba cha mtihani.


“sisi kama Nicopolis academy na Ludewa education centre tumeona tutoe mchele huu kidogo kwa shule za kata ya Ludewa,tunaomba na wadau wengine watuunge mkono kwani uwezo wa wazazi umetofautiana,mwingine anamuahidi mtoto wake atamletea chipsi hivyo mtoto akiwa darasani atashindwa kufanya mtihani akibaki na mawazo kuwa leo lazima niwaoneshee wezangu kwa kula chipsi hivyo kwa chakula cha pamoja haitatokea hilo,”alisema Mwalimu Mwinuka.


Alisema kuwa Nicopoli Academy inawafadhiri hivyo ikaona ufadhiri huo ni vyema shule nyingine zikanufaika kwani Mwalimu Mwinuka aliahidi kutoa usafiri kwa wanafunzi wa shule ya msingi Songambele waishio Ngalawale kwa kipindi hiki cha mtihani kwani wamekuwa wakitembea umbali mrefu unaokadiriwa kilometa 6 hadi shuleni hapo.


Aidha akishukuru kwa msaada huo mratibu wa Elimu kata ya Ludewa Mwalimu Lenis Mtitu alivipongeza vituo hivyo kwa kuona umuhimu wa kuwasaidia chakula wanafunzi wa darasa la saba hasa kipindi cha mitihani kwani ni ukweli usiopingika uwezo wa kifamilia haulingani hivyo wata wazazi wanapowaletea watoto wao chakula kipindi hiki lazima utofauti utatokea.


Mwalimu Mtitu alisema kuwa kama jamii na wadau mbalimbali wataelimishwa nini wanatakiwa kukifanya kwa watoto wao kipindi cha mitiahani basi hata ufaulu unaweza kuongezeka kutokana na hali halisi za kifamilia kwa kuna wanafunzi wengine hushindwa kurudi majumbani mwao mchana kupata chakula huvyo hulazimika kukaa na njaa wakisybiri mtiahani.


Hata hivyo Mratibu elimu kata huyo alivitaka vituo hivyo kuendeleza tabia hiyo na kuwataka wadau wengine wa elimu kuiga mfano huo ambao unaleta tija katika sekta ya elimu ikiwa pamoja na kuongeza ufaulu kwa wanafunzi.


Mwisho.

No comments: