Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

August 16, 2017

DC LUDEWA AKABIDHI AHADI YA WAZIRI MKUU KWA TIMU YA MAPINDUZI QUENS FC.

 Mh.Andrea Tsere akimkabidhi Jezi Matron wa Mapinduzi Quens fc Bi.Evelina Mgaya
 Mh.Andrea Tsere akimkabidhi Jezi Kocha wa Mapinduzi Quens Fc Bw.Hilaly Lugome

Matha Luoga akikabidhiwa jezi na mkuu wa wilaya ya Ludewa Mh.Andrea Tsere


Mkuu wa wilaya ya Ludewa Mh.Tsere akiongea na wananchi pembeni yake ni mshauri wa mgambo wa wilaya ya Ludewa
 Mh.Andrea Tsere akimkabidhi Jezi Matron wa Mapinduzi Quens fc Bi.Evelina Mgaya
Bi.Zaina Mlawa katibu tawala wa wilaya ya Ludewa akikadhi jezi tayari kwaajili ya kuukabidhi uongozi wa Mpinduzi Quens Fc
 Mkuu wa wilaya ya Ludewa Mh.Tsere akiongea na wananchi
 Evelina Mgaya akiwa pamoja na baadhi ya wachezaji

 Mh.Tsere akiongea na baadhi ya vijana wanaopata mafunzo ya Mgambo
  Mh.Tsere akiongea na baadhi ya vijana wanaopata mafunzo ya Mgambo


  Mh.Tsere akiongea na baadhi ya vijana wanaopata mafunzo ya Mgambo


Mkuu wa wilaya ya Ludewa katika mkoa wa Njombe Mh.Andrea Tsere ameikabidhi rasmi timu ya mpira wa miguu wasichana ya wilayani Ludewa ya Mapinduzi Quens fc jezi ambazo waliziomba kwa Waziri mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Majaliwa Kassim Majaliwa  wakati wa ziara yake iliyafanyika wilayani hapa.

Akikabidhi jezi hizo jana katika uwanja wa mpira wa miguu wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa Mh.Tsere alisema kuwa Waziri mkuu ni mdau wa michezo na anatambua umuhimu wa michezo hivyo ametimiza ahadi yake aliyoihaidi kwa timu hiyo hivyo kwa kuonesha umuhimu wa mchango wake katika timu ya mpira wa miguu wasichana wilaya ya Ludewa ni vyema kuiendeleza timu hiyo ili ifanye vizuri katika mashindano ya mkoa na Taifa.

Alisema kuwa Mh.Mjaliwa ameanza kuwa kuisaidia Jezi lakini wadau mbalimbali ikiwa pamoja na wanaludewa wanatakiwa kuisaidia timu hiyo kwani bado inaupungufu mkubwa wa vifaa vya michezo hivyo kama yeye mkuu wa wilaya aliahidi kuichangia Mapinduzi quens mipira miwili ili iendelee na mazoezi ya kila siku.

“Mh.Majaliwa ametuunga mkono kwa kutupatia Jezi lakini sisi kama wanaludewa tunatakiwa kuhakikisha timu yetu inasonga mbele kwani wilaya yetu inavipaji vya kutosha hivyo haina sababu ya kuvipoteza vipaji hivi zaidi ya kuviendeleza kinachotakiwa ni kuungana na mwalimu wa timu hii pamoja na uongozi wao kuifikisha pahala”,alisema Tsere.

Awali akitoa shukrani kwa Waziri mkuu kwa kutoa msaada wa jezi hizo mwalimu wa Timu hiyo Bw.Hilaly Lugome alisema kuwa timu hiyo ambayo imepata sale kutoka kwa Mh.Majaliwa bado inachangamoto nyinge katika msimu huu ambao inatakiwa kushiriki ligi ya mkoa.

Bw.Lugome alimshukuru waziri mkuu kwa kuijali michezo na kwa kukamilisha ahadi yake ambayo aliahidi katika mkutano wa hadhara hivyo bado wadau wanatakiwa kumuunga mkono waziri mkuu kwa kuisaidia timu hiyo katika vifaa vingine vya michezo ikiwa pamoja na viatu mipira na chakula kwaajili ya kambi.

Tukio hilo la ugawaji wa jezi lilifanyika sambamba na ufunguzi wa mafunzo ya jeshi la akiba la mgambo kwa kata ya Ludewa ambapo jumla ya vijana 42 wamejitolea kwa hiyari yao kupata mafunzo hayo.

Mwisho.

No comments: