Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

May 02, 2017

TAZARA YAMUOMBA RAIS MAGUFULI KUZUIA MIZIGO MIZITO INAYOBEBWA NA MAROLI KWANI YANAHARIBU MIUNDOMBINU YA BARABARA.

Mgeni rasmi Mh.Christopher Ole Sendeka akiongea na wafanyakazi wilayani Ludewa
Mh.Sendeka akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi
Ngoma ya Asili ya Mganda kutoka kata ya Lupingu ikitumbuiza katika sherehe za wafanyakazi


Mh.Sendeka akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi 

Mh.Sendeka na viongozi wa vyama vya wafanyakazi wakiwa pamoja na waandishi wa habari
Mh.Sendeka akipata maelekezo kutoka kwa meneja wa kituo cha radio cha Best fm Bwana Godluck Mshairi kilichopo wilaya ya Ludewa katika mabanda ya maonesho ya Meimosi wilayani Ludewa
Idara ya maendeleo ya jamii wakitoa maelekezo kwa Mh.Sendeka




Tazara imemuomba Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuri kuzuia ubebwaji wa mizigo mizito unaofanywa na magari ya mizigo kutoka bandari ya Dar es Salaam kuelekea nchini Zambia kunafanya Treni za mizigo za reli hiyo kukosa mizigo na pia magari hayo yanachangia uharibufu wa miundombinu ya barabara hali inayoitia hasara Serikali ya Tanzania.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mwalimu Fratern Kwahhison katibu wa kamati ya meimosi na katibu wa CWT Mkoa wa Njombe kwa Mgeni rasmi wa Serehe za Mei mosi mkoa wa njombe ambaye ni mkuu wa mkoa huo Mh.Christopher Ole Sendeka sherehe ambayo kimkoa ilifanyika wilaya ya Ludewa na kudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka katika wilaya za mkoa wa Njombe pia wananchi wa wilaya ya Ludewa.

Akisoma risala hiyo Mwalimu Kwahhison alisema kuwa sheria iliyopo inayosimamia taasisi ya Tazara inayoitwa Tazara ACT,haiendani na hali halisi,serikali ya Tanzania na ile ya Zambia iangalie upya sheria hii ili ilete tija kwani Tazara imekuwa ikishindwa kufanya biashara hasa katika mizigo kutokana na mizigo mingi mikubwa kubebwa na magari hali inayoifanya Tazara kushindwa kujiendesha.

Alisema kubwa magari hayo makubwa ya mizigo yamekuwa ndio chanzo cha uharibifu wa barabara kutokana na uzito mkubwa na kuitia hasara Serikali ya Tanzania kuwa na bajeti ya matengenezo ya barabara kila mwaka hivyo ni vyema mizigo hiyo inngesafirishwa kwa kutumia reli ya Tazara ili kuinusuru miundombinu ya barabara.

Katika risala hiyo pia Mwalimu Kwahhison aliitaka Serikali kuangalia  malimbikizo ya walimu na kuyalipa kwa wakati ikiwa pamoja na upandishwaji wa madaraja kwani kimekuwa kilio cha muda mrefu kisichotekelezeka ikiwa na upungufu mkubwa wa wafanyakazi wa sekta ya Afya hasa vijijini,kushushwa vyeo vya ngazi ya mishahara kwa maafisa Tarafa kutoka TGS F 5 hadi TGS 0 badala ya kubaki TGS 5 na kutolipwa malimbikizo ya mishahara yao toka 2012 hadi sasa.

Alisema kuwa Mkoa wa Njombe ni miongoni mwa mikoa isiyo na Mahakama ya Rufaa na ni mikoa ambayo inakua kwa kasi kwa kuwa na raslimali nyingi zinazovutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi,hali hii inasababisha matukio mengi ya kiuharifu kuongezeka kutokana na mwingiliano mkubwa wa watu hivyo Serikali inaomba kulitatua tatizo hilo mapema.

Akitoa Hotuba katika sherehe hizo mkuu wa mkoa wa Njombe Mh.Christopher Ole Sendeka ambaye ndio Mgeni Rasmi alisema kuwa Serikali ya awamu ya tano iko makini kuhakikisha maslahi ya wafanyakazi yanaboreshwa hivyo baadha ya zoezi la kuwatambua watumishi hewa neema inakuja kwa wafanyakazi waadirifu na wachapakazi.

Mh.Sendeka alisema kuwa kuhusuana na suala la Tazara litapatiwa ufumbuzi hivyo malalamiko hayo tayari Mh.Rais anayo,pia kuhusiana na mkoa wa Njombe kukosekana kwa Mahakama ya Rufaa ni kweli jambo hilo bado mkoa wa Njombe unatumia Mahakama ya Iringa kutokana na ukweli kwamba mkoa wa Njombe ulitokana na Mkoa wa Iringa hivyo taratibu zinaendelea kufanyika kujiondoa taratibu ktk mkoa Mama.

Alisema kuwa mamlaka nyingi zilikuwa bado Iringa lakini taratibu Serikali imezihamisha na kuwa Njombe kama mkoa hivyo hata hili la Mahakama ya Rufaa itafanyiwa kazi,pia aliwataka wafanyakazi kutokuwa wanyonge kwani ofisi yake iko wazi muda wote na kama kuna kero inayohusu wafanyakazi basi vyama vya wafanyakazi visisite kumuona ili kutatua kero hizo.

Mwisho.
 
KWA UDHAMINI WA MTANZANIA RESTAURANT, WANAPATIKANA LUDEWA MJINI KATIKA JENGO LA NDICHELIWE.

 KWA CHAKULA SAFI NA BORA UKIFIKA LUDEWA MJINI MTANZANIA RESTAURANT NDIO SURUHISHO PIA KWA CHAKULA CHA MAHARUSI,MISIBA MAHAFARI NA SHEREHE MBALIMBALI
 KWA MAWASILIANO PIGA NO.0758146258 au 0624985168 KWA CHAKULA CHA UHAKIKA.


No comments: