Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

March 25, 2015

KILELE CHA SIKU YA MAJI DUNIANI KIMKOA CHAFANYIKA WILAYANI LUDEWA KATIKA KIJIJI CHA MUHOLO






mkuu wa mkoa akisomewa taarifa na viongozi wa wilaya ya Ludewa





mkuu wa mkoa wa Njombe Dkt.Rehema Nchimbi akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Muholo
Mkuu wa wilaya ya Ludewa Bw.Anatory Choya



Wiki ya maji duniani katika mkoa wa Njombe ilifanyika wilayani Ludewa katika kijiji cha Muholo kata ya Luana ambapo mkuu wa mkoa wa Njombe Dkt.Rehema Nchimbi aliweza kufanya uzinduzi wa mradi wa maji katika kijiji hicho uliojengwa na wafadhiri kwa kushirikiana na Halmashauri ya wilaya ya Ludewa.


Akizindua maradi huo Dkt.Nchimbi umegharimu kiasi cha shilingi 150 milion aliiagiza Halmashauri ya wilaya ya Ludewa  kubuni miradi ya maji ambayo itawasaidia wananchi kwa muda mrefu kwani kwa kushirikiana na wafadhiri tatizo la ukosefu wa maji safi na salama katika wilaya linaweza kupungua kama si kuisha kabisa.


Mradi huo mkubwa uliozinduliwa na mkuu wa mkoa umefadhiriwa na Shirika la Manos Unidas la nchini Hispania na kutekelezwa na Asasi ya Youth Rural Development Association (YORDA) ambao unauwezo wa kuwahuduma wananchi wa kijiji hicho kwa zaidi ya miaka kumi kutokana na uwingi wao.

No comments: