Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

February 24, 2015

WAZEE LUDEWA WACHOSHWA NA MFUMO WA KUBADIRI VIONGOZI KILA KIPINDI CHA UCHAGUZI. WAMTAKA FILIKUNJOMBE KUENDELEA KUIONGOZA LUDEWA MIAKA MINGINE MITANO



Wazee wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe wameendelea kusisitiza kuwa wamechoshwa na tabia iliyojengeka kwa wananchi wa wilaya hiyo ya kubadiri viongozi hasa kwa upande wa nafasi ya ubunge kila kipindi cha uchaguzi hivyo wanamtaka mbunge wa sasa wa jimbo hilo Deo Filikunjombe kuchukua fomu na kuendelea kuliongoza kwa kipindi kingine cha miaka mitano.

Akiongea hivi karibuni na mwandishi wa habari hii mwanasiasa mkongwe wilayani hapa ambaye amewahi kuwa diwani wa kata ya Ludewa mjini na baadae kuwa mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa kwa muda wa miaka 10 na kuamua kuachana na siasa Mzee Hilali Nkwera alisema kuwa ni tabia iliyozoeleka kwa wananchi kubadiri viongozi kila kinapofika kipindi cha uchaguzi hali ambayo inarudisha maendeleo ya wilaya nyuma.

Mzee Nkwera alisema katika historia ya wilaya ya Ludewa ni mbunge mmoja pekee ndiye aliyewahi kudumu katika madara yake kwa muda wa miaka 25 ambaye ni hayati Mathias Kihaule lakini tangia alipochukua utawala huo hayati Horace Kolimba imekuwa ni mabadirishano ya kila kipindi hali ambayo ni mbaya kwa maendeleo kwani mikakati ya kimaendeleo haiwezi kufanikiwa kwa muda wa miaka mitano.

Alisema kuwa Filikunjombe ameanza kufanya maendeleo kwa kasi kubwa hivyo hapaswi kupingwa zaidi ya kuungwa mkono kwa yale anayoyafanya kwani wananchi wa wilaya ya Ludewa hawana haja na mtu mwingine wa kuliongoza jimbo hilo zaidi yake ambaye kupitia Serikali ameweza kuibadiri wilaya kwa muda mfupi ambao amekuwa kiongozi.

“Sisi kama wazee wa wilaya ya Ludewa hatuna haja ya mbunge mwingine kwani anayoyafanya mtoto wetu Deo Filikunjombe tunayaona na ametuletea sifa kubwa nchini kuwa kumchagua yeye ambaye ni mchapa kazi,wako vijana wanaokuja kutuomba tuwape nafasi na tumewajibu wamuache mwezao aendelee na mipango aliyoianza kuitekeleza ili wilaya ibadirike zaidi tofauti na zamani na nataka kuwaeleza wananchi kuwa tumeamua kuacha tabia ya kubadirisha wabunge kila mwaka kwani tumeziona athari zake za kurudi nyuma kimaendeleo”,alisema Mzee Nkwera.

Mzee Nkwera alisema kuwa kila anapochaguliwa mbunge mwingine huanza na mipango yake ya maendeleo lakini kabla haja maliza utekelezaji tayari kipindi cha miaka mitano kinakuwa kimekwisha hivyo wilaya inabaki nyuma na kupitwa na wilaya za jirani licha ya kuwa wilaya ya Ludewa ni moja kati ya wilaya tajiri nchini.

Nae Bi.Gerewada Nyandoa alisema kwa upandewa wakina mama hawanashida na utendaji wa Filikunjombe kwani ameweza kuwasaidia katika maendeleo ya ujenzi wa Zahanati ambazo ni mkombozi kwa mwanamke wakati kabla ya ujenzi wa Zahanati hizo 3 wanawake walikuwa wakitembea umbali mrefu kwaajili ya kufuata huduma.

Bi.Gerewada alisema hivi karibuni wazee wa kijiji cha Nsele kata ya Kilondo walitoa fedha taslimu shilingi laki moja na kumkabidhi Filikunjombe ili aweze kujiandaa kuchukua fomu ya kugombea Ubunge,fedha hizo ziliwakilisha wazee wote wa wilaya ya Ludewa ambao wanadhamira ya kunufaika na kushuhudia maendeleo yanayoletwa na kijana wao ambaye walimpigania kuchukua nafasi hiyo kwa manufaa ya wilaya na Taifa.

Aidha Mzee George Kilongo anayewakilisha wazee wa mwambao wa ziwa nyasa aliusifu utawala wa Filikunjombe kuwa ni utawala wenye neema kwani ni mbunge ambaye ameweza kutembelea vijiji vyake vyote vya ziwa nyasa ndani ya miaka mitano licha ya kuwa kuna baadhi ya vijiji huwezi kufika kwa kutumia gari wala boti zaidi ya kutembea kwa miguu kwa muda wa masaa 5 hali ambayo imewashangaza wananchi kuona mbunge huyo akifika na msafara wake.

Mfano wa vijiji hivyo vyenye mazingira magumu ya kufikika ni kijiji cha Liunji,Kimata na Nkwimbili ambako hakuna mbunge ambaye aliwahi kifika lakini Filikunjombe ameweza kuvitembelea na kutoa misaada ya Afya,Elimu na maji hali ambayo imewafanya wananchi wa vijiji hivyo kuona kuwa mbunge huyo anapaswa kuendelea kuiongoza wilaya ya Ludewa kwa muda mrefu ili kuendelea kuwasaidia wananchi.

Mzee Kilongo alisema kila utawala unaneema zake kutokana na utendaji wa Filikunjombe pia alielekeza pongezi kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Prof Jakaya Mrisho Kikwete katika utawala wake kwa kuweza kuleta maendeleo katika vijiji visivyo fikika kwa kupitia Filikunjombe.


Mwisho.

No comments: