Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

June 23, 2014


SERIKALI WILAYANI RUNGWE NA KYELA ZATEKETEZA BIDHAA HARAMU ZA TSH,MIL.90

Na Ibrahim Yassin,Rungwe

SERIKALI wilayani Rungwe mkoani Mbeya imeteketeza kwa kuvichoma moto vipodozi venye viambata vya sumu pamoja na pombe haramu za viroba tani 380 vyenye thamani ya Tsh mil,80 vilivyokuwa vinaingizwa nchini kutoka Malawi na wafanyabiashara wasio waaminifu kwa lengo la kujiingizia kipato huku wakiharibu maisha ya watanzania waliokuwa wakizitumia pombe hizo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana mara baada ya uchomaji huo mkuu wa wilaya hiyo Chrispin Meela alisema kuwa vipodozi na pombe hizo walizikamata katika operesheni iliyofanyika mwanzoni mwa mwaka 2013 hadi mwezi april mwaka 2014 katika msako ulioendeshwa na kikosi kazi cha kamati ya ulinzi na usalama pamoja na maafisa wa TFDA na TRA na kufanikisha zoezi hilo.

Alisema wafanyabiashara wasio waaminifu wamekuwa wakivusha vipodozi hivyo kutoka nje ya nchi kwa njia za panya zilizopo mipakani, na kwa upande wa pombe kali za viroba toka Zambia na Malawi wamekuwa wakipitisha kwenye mpaka wa Kasumulu boda kwa njia za panya zilizogunduliwa kuwa ni 32 na kuzipeleka mikoani kwa ajiri ya kuziuza huku wakifahamu kuwa bidhaa hizo ni haramu na hazijadhibitiswa.

Meela aliongeza kuwa amewaagiza askari wa usalama barabarani wawe makini kukagua bidhaa hizo ambazo kwa sasa aina mama wamekuwa wakipakatia mithiri ya mtoto mchanga na kuwa bidhaa hizo zimekwisha poteza maisha ya watanzania wengi na wengine wamekwisha haribikiwa hivyo Taifa limekuwa likipoteza nguvu kazi hasa kwa vijana.

Aliongeza kuwa kwa sasa watatumia sheria za TRA pindi watakapo kamata bidhaa hizo watataifisha bidhaa pamoja na gari badara ya ile sheria ya TFDA ya kutoza faini pindi wanapo kamata bidhaa haramu ambayo haijadhibitiswa na kuwa wameamua kufanya hivyo ili kuhakikisha bidhaa hizo hazitumiki tena na badala yake zitumike bidhaa za kitanzania ambazo zimedhibitishwa na shirika la viwango nchini TBS.

Kwa upande wa wilaya ya Kyela Serikali ya wilaya hiyo imeteketeza na kuchoma moto bidhaa hizo zenye thamani ya Tsh,mil,1.2 huku mkuu wa wilaya hiyo Magret Malenga akitoa msisitizo kwa vijana kuacha kuzitumia bidhaa hizo kwa madai kuwa zinamadhara makubwa yanayoweza kuwapata pindi watumiapo.

Malenga alisema kuwa bidhaa zingine bado hazijachomwa kwa kuwa bado zina kesi ambazo zinaendelea mahakamani na kwamba ameiagiza idara husika kufanya doria maeneo yote hasa katika njia hizo 32 za panya zinazotumika kuvushia bidhaa hizo na watakapo mkamata mtu na bidhaa hizo wataitahifisha na mwenyebidhaa atafikishwa mahakamani.

Meneja wa mamlaka wa chakula na dawa kanda ya kusini Rodney Alananga alisema kuwa baada ya kukithiri kwa uingizwaji wa bidhaa hizo alitoa taarifa kwa mkuu wa mkoa Abbas kandoro ambaye aliitisha kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa na kuwaagiza wakuu wa wilaya kuanzisha msako huo ambao umezaa matunda na uigizwaji na uuzaji wa bidhaa hizo umepungua kwa asilimia 80.

Alananga alisema kuwa TFDA imewapa meno kamati za ulinzi na usalama zilizo chini ya wakuu wa wilaya kwa kushirikiana na maafisa wa TRA kuhakikisha wanaendelea na zoezi hilo ili kuhakikishwa wanafanikiwa kuzitokomeza bidhaa hizo huku watanzania wakiendelea kuwa salama kwa kuzitumia bidhaa zilizo salama zilizodhibitiswa na shirika la viwango n chini yaani TBS.
Mwisho.
0767269996

No comments: