Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

October 17, 2012

WAZIRI WASSIRA ASHANGAZWA KUONA ZAIDI YA WANAFUNZI 2000 WASIOJUA KUSOMA NA KUANDIKA



Na Nickson Mahundi,Ludewa

Waziri wa nchi ofisi ya Rais mahusiano na Uratibu Mh.Steven Wassira ameshangazwa na ripoti ya wilaya ya  Ludewa Mkoani Njombe iliyosomwa na mkuu wa wilaya hiyo Bw.Juma Madaha kuwa zaidi ya wanafunzi elfu mbili hawajui kusoma wala kuandika.

Taarifa hiyo imesomwa wakati wa ziara ya Waziri Wassira wilayani Ludewa katika kukagua miradi ya kimaendeleo inayosimamiwa na TASAF THREE pamoja na MKURABITA ambapo ziara hiyo ilianzia katika shule ya sekondari Luana na itaendelea kesho.

Katika taarifa yake mkuu wa wilaya ya Ludewa Bw.Madaha alizitaja changamoto wanazokabiliana nazo kwa upande wa elimu ni pamoja kuwa na wanafunzi zaidi ya elfu mbili wasiojua kusoma na kuandika wakati juhudi za kulimaliza tatizo hilo zinaendelea.

Hali hiyo ilimfanya Waziri Wassira kushikwa na mshangao ambapo ilimpasa kumuuliza mtoa taarifa kuwa hao wisiojua kusoma nakuandika kwanakwendaje katika shule za Sekondari na inakuwaje wahitimu elimu ya msingi kwa hali hiyo.

Bw.Mdaha alijibu kuwa  kutokana naukosefu wa walimu unaoikumbu wilaya hiyo ndio sababu kubwa zinazofanya wanafunzi wafikie hatua hiyo lakini uongozi wa wilaya umepanga mipango ya kulimaliza tatizo hilo.

“tatizo hilo tunalo lakini tumeandaa mpango wa kuwashawishi vijana wanaohitimu kidati cha nne kwa masharti maalumu kuwapeleka katika vyuo vya elimu ili wamalizapo masomo yao warudi kufanya kazi katika shule zetu”,alisema Bw.Madaha.

Adha mradi wa TASAF umetumia zaidi ya shilingi za kitanzania milioni 42 katika ujenzi wa vymba vya madarasa,jingo la utawala pamoja na ujenzi wa matundu manne ya choo katika shule ya Luana ambapo ukarabati  wa majengo hayo umeshamalizika.

Akitoa hotuba yake Mh.Wassira alisema Serikali imeamua kuungana na wananchi katika kuleta maendeleo vijijini kwa kutoa fedha lakini kinachotakiwa wananchi wenyewe wanapaswa kuibua miradi na kuiombea fedha.

Alisema fedha za TASAF hutumika kununulia mahitaji ya viwandani katika ujenzi lakini wananchi huchangia nguvu kazi ili kupata mafaniko ya miradi mbalimbali nchini kwani nchi hujengwa na wananchi wenyewe.

Aidha aliwataka vijana wa wilaya hiyo kuunda vikundi vitakavyowawezeshz kujiajiri katika kilimo cha matunda na mbogamboga ambapo wataweze kazisafirisha bidhaa zao kutoka wilayani Ludewa hadi kiwanja cha ndege Songwe Mbeya na kuuza nje ya mkoa.

Ziara hiyo inatarajia kuendelea katika Kijiji vya Shaurimoyo kata ya Lugarawa na Kijiji cha Amani kata ya Mundindi ambako kunamiradi ya TASAFU na katika kijiji cha Amani Mh.Wassira anatarajia kukabidhi hati za Ardhi za Kimila kwa wananchi na kufanya mkutano wa Hadhara na baadae atarudi mkoani Njombe.

Mwisho

No comments: