Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

October 21, 2012

NDC YAZINDUA MRADI WA PAACA WA KUWASHIRIKISHA WANANCHI WA WILAYA YA LUDEWA KATIKA UCHIMI


Na Nickson Mahundi,Njombe

Shirika la Maendele la taifa(NDC) kupitia mradi wake wa PAACA limeanza kutoa elimu kwa wananchi wa wilaya ya ludewa namna ya kujikwamua kiuchumi na kuweza kuuza mahitaji mbalimbali yanayotakiwa na wawekezaji wa migodi ya Mchuchuma na Liganga.

Akizungumza katika ufunguzi wa mradi huo mwezeshaji wa kitaifa wa mradi huo Bw.Deosdedis Mtambalike alisema mradi huo utakuwa wakwanza katika Afrika Mashariki kwani katika Afrika ni nchi ya Afrika ya kusini ndio iliweza kuwaandaa wananchi wake kupitia mradi huo.

Bw.Mtambalike alisema Mradi wa PAACA unalengo la kuonesha namna ya kuwashirikisha wananchi wa kawaida kiuchumi ili waweze kuiona miradi hiyo mikubwa ni mali yao na si vinginevyo kutokana na ajira na kujiajiri kutakakotokea eneo hilo.

Alisema wilaya ya Ludewa ina fulsa nyingi hivyo wananchi wanatakiwa kuelimishwa namana ya kuzitumia filsa hizo kwani wasipowezeshwa watabaki kuwa watazamaji kwa wageni watakonufaika na migodi hiyo.

“NDC imeona ni vema kuwaandaa wananchi wa wilaya ya Ludewa kwani wawekezaji wanahitaji mahitaji mbalimbali yakiwemo mahitaji ya chakula na vifaa vya ujenzi hivyo mradi wa PAACA umeanzia Ludewa na utaenea maeneo mengine ya migodi nchini”,alisema Bw.Mtambalike.

Awali mkurugenzi wa NDC wa Viwanda mama Bw.Aley Mwakibolwa alisema miradi mingi ya migodi hutoa kodi tu Serikalini hivyo wananchi wanatakiwa kushiriki kikamilifu katika migopdi ili kujiletea maendeleo kwa kujiajiri na kuajiriwa.

Bw.Mwakibolwa alisema NDC imejipanga kwa kusambaza elimu ya kujianda na ujio wa wageni wa migodi ili wananchi waweze kuwa na maisha bora kwa kuwatoa wataalamu kutoka Ufaransa na maeneo mengine.

Alisema kampuni ya wachina imeainisha mahitaji wanayotaka kutoka kwa wananchi mahitaji hayo ni Unga,Matunda,Mboga za majani,Vitunguu vya aina zote,Samaki pamoja na Nyama hasa ya Nguruwe kwa muda wote watakao fanya kazi katika migodi hiyo.

Bw.Mwakibolwa aliwataka wananchi wa wilaya ya Ludewa kuchukua hatua kupitia elimu watakayoipata katika mradi wa PAACA kuyaandaa mahitaji hayo ambayo yatawaptia kipato wananchi hao ambachokitawasaidia kuondokana na umaskini uliokithiri.

Aidha Mkuu wa wilaya ya Ludewa Bw.Juma Madaha ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo alilishukuru shirika la maendeleo la Taifa (NDC) kwa kuuleta mradi huo wilaya kwake kwa mara ya kwanza Afrika Mashariki katika kuishirikisha jamii.

Bw.Madaha alisema wananchi wa wilaya yake wako tayari kwani wanatambua kuwa wanafulsa nyingi lakini walikuwa hawajui kipi cha kuanza nacho lakini kwa kupitia mradi huo watakuwa na jibu la nini kifanyike.

Mwisho.

No comments: