Mwnyekiti wa mradi wa champion mkoa wa Iringa Bw.Mlongwa
Rojas Mkuchu amefariki Dunia leo asubuhi katika hospitari ya Ocen Road jijini Dar es salaam alikokuwa
akitibiwa
Meneja wa kituo cha radio Nuru Fm Bw.Victor
Chakudika ameuarifu mtandao huu wa www.habariludewa.blogsport.com
kuwa aliyepata kuwa mwandishi wa shirika la IDYDC katika ukusanyaji wa
habari za vijana ,shirika ambalo linamiliki kituo hicho cha Radio Nuru Fm
Mlongwa Mkuchu amefariki dunia leo asubuhi katika Hospitali ya Ocen Road jijini
Dar es Salaam ambako alikuwa akitibiwa .
Bw.Mlongwa aliwahi kufanya kazi pia kwa karibu kama mratibu wa ukimwi katika shirika la IDYDC na hayati.Philoteus Njuyuwi kuanzia mwaka 2004 hadi mwaka 2007 ndipo aliachana na kazi hiyo na kuingia katika miradi mingine mkoani iringa.
Bw.Mlongwa aliwahi kufanya kazi pia kwa karibu kama mratibu wa ukimwi katika shirika la IDYDC na hayati.Philoteus Njuyuwi kuanzia mwaka 2004 hadi mwaka 2007 ndipo aliachana na kazi hiyo na kuingia katika miradi mingine mkoani iringa.
Atakumbukwa kwa mengi kutokana na utendaji wake wakazi
kutokana na kuweza kuzitembelea wilaya zote za mkoa wa Iringa ikiwemo wilaya ya
Ludewa kutokana na elimu yake kama muwezeshaji
wa mafunzo mbalimbali katika jamii.
Taarifa zinaeleza kuwa alikuwa akisumbuliwa na tatizo la
ugonjwa wa kansa katika mgongo wake kwa miaka miwili na kupelekwa katika
Hospitali hiyo.
Mbali ya mchango wa Mlongwa kuwa mkubwa katika jamii enzi za uhai wake bado Mlongwa atakumbukwa kwa mambo mbali mbali ya kijamii ambayo amepata kuyafanya enzi za uhai wake katika kuielimisha jamii ya mkoa wa Iringa juu ya janga la UKIMWI kupitia mradi wa WANAUME TUWAJIBIKE .
Kwa wadau wa mtandao huo msiba wa Mlongwa pia ni pigo kubwa kutokana na mchango mkubwa ambao mke wake Jamida Kulangwa ambao aliutoa kwa mtoto Juliana Mwinuka wa kijiji cha Mavanga Ludewa ambaye aliungua kwa moto na kuendelea kutaabika nyumbani kwa zaidi ya miezi sita bila kusaidia hadi mwanamke huyo Jemida alipofikisha taarifa zake katika mtandao huu na kuanza kusaidia kabla ya kwenda kijijini kumfuata mtoto huyo kwa kushirikiana na msamaria mwema mmoja mkazi wa jiji la Dar es Salaam na mkazi wa Ludewa walikubali kujitolea kuacha shughuli zao na kwenda kumchukua mtoto huyo .
Hadi leo Jemeda anapatwa na tatizo hilo ndie alikuwa msaada mkubwa wa kumuuguza mtoto huyo akishirikiana na mdau huyo mkazi wa jiji la Dar es Salaam na Jemida alikuwa akimuuguza mtoto Juliana katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili aliko sasa huku akiendelea pia kumuuguza mume wake katika Hospitali ya Ocen Road hadi kifo kinapomkuta.
Mtandao huu unaendelea kumpa moyo mdau Jemida Kulangwa kupiga moyo konde katika kipindi hiki kizito kwake na kuwaomba wadau kuendelea kumsaidia mtoto Juliana Mwinuka pia.
Mbali ya mchango wa Mlongwa kuwa mkubwa katika jamii enzi za uhai wake bado Mlongwa atakumbukwa kwa mambo mbali mbali ya kijamii ambayo amepata kuyafanya enzi za uhai wake katika kuielimisha jamii ya mkoa wa Iringa juu ya janga la UKIMWI kupitia mradi wa WANAUME TUWAJIBIKE .
Kwa wadau wa mtandao huo msiba wa Mlongwa pia ni pigo kubwa kutokana na mchango mkubwa ambao mke wake Jamida Kulangwa ambao aliutoa kwa mtoto Juliana Mwinuka wa kijiji cha Mavanga Ludewa ambaye aliungua kwa moto na kuendelea kutaabika nyumbani kwa zaidi ya miezi sita bila kusaidia hadi mwanamke huyo Jemida alipofikisha taarifa zake katika mtandao huu na kuanza kusaidia kabla ya kwenda kijijini kumfuata mtoto huyo kwa kushirikiana na msamaria mwema mmoja mkazi wa jiji la Dar es Salaam na mkazi wa Ludewa walikubali kujitolea kuacha shughuli zao na kwenda kumchukua mtoto huyo .
Hadi leo Jemeda anapatwa na tatizo hilo ndie alikuwa msaada mkubwa wa kumuuguza mtoto huyo akishirikiana na mdau huyo mkazi wa jiji la Dar es Salaam na Jemida alikuwa akimuuguza mtoto Juliana katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili aliko sasa huku akiendelea pia kumuuguza mume wake katika Hospitali ya Ocen Road hadi kifo kinapomkuta.
Mtandao huu unaendelea kumpa moyo mdau Jemida Kulangwa kupiga moyo konde katika kipindi hiki kizito kwake na kuwaomba wadau kuendelea kumsaidia mtoto Juliana Mwinuka pia.
BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE
No comments:
Post a Comment