Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

October 17, 2012

MAZISHI YA MLONGWA YAZUA UTATA NDUNGU UPANDE WA BABA NA MAMA WAVUTANA


Utata mkubwa umezuka katika msiba wa marehemu Robert Mlongwa baada ya pande mbili za marehemu kuvutana kuhusu atakapozikwa marehemu.

Akizungumza na mtandao huu ndugu mmoja wa marehemu ambaye hakutaka kutaja jina lake ameeleza mwili wa marehemu ulifika alfajiri ya leo ukitokea Dar es salaam alipokuwa akitibiwa marehemu, na kufikia nyumbani kwa baba yake marehemu kwa jina  Mchungaji Mkuchu.

Baada ya hapo baba huyo wa marehemu alikataa mwili wa marehemu usisafirishwe Tanangozi ambapo ndipo mama wa marehmu alipozikwa, ambapo pia kumekwisha andaliwa shughuli za maziko na kuamuru kuwa mwili huo utazikwa katika makaburi ya mtwivila.

Mpaka mtandao huu unatoka eneo la tukio hakuna muafaka ulikuwa umefikiwa huku baba wa marehemu akiwa amejifungia chumbani.

No comments: