Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

October 17, 2012

LIJUE SHILA LA LUDENDE DEVELOPMENT ASSOCIATION(LUDA)


 IJUE ASASI YA LUDA
 
Ludende Development Association ni Asasi ya kiraia iliyosajiriwa kufanya kazi kiataifa, yenye namba ya usajiri wa 00NGO/ 1211, yenye makao yake makuu katika Kijiji cha Ludende Wilayani Ludewa, Mkoani Njombe. Asasi hii ilianzishwa mwaka 2005 ikiwa na wanachama waanzilishi watano.

Asasi hii ilianzishwa ikiwa na madhumuni ya msingi kama yafuatayo:-
Kuhifadhi vyanzo vya maji na mazingira vijijini  na kuzuia uharibifu wa Mazingira.

Kuhamasisha wanachama na jamii juu ya umuhimu wa kuanzisha vyama vya Akiba na Mikopo (SACCOS

Kuongeza uelewa wa kisheria kwa watu masikini na watu wanaoishi katika mazingira magumu.

Kulinda na kutetea haki za binadamu, Utawala bora, na kufuatilia wajibu wa Serikali kwa jamii.

Kusaidia wanawake, vijana na watoto yatima kwenye masuala ya kijamii na kiuchumi.

Kupambana na kudhibiti kilimo na matumizi ya Madawa ya kulevya.

Kutunza na kutoa misaada mbalimabali kwa watu wanaoishi na VVU/Ukimwi.

Kulinda, kuhamasisha na kuendeleza mawazo ya watu kama shughuli za mikono, ngoma na miziki ya asili.
Pamoja na malengo yote hayo tumejitahidi kutimiza sehemu ya hayo malengo kwa kila tulipopata fursa ya kufanya hivyo kama ifuatavyo:-

Tumefanya miradi ya uhamasishaji wa jamii juu ya uhifadhi wa mazingira kwa kupanda miti kwenye vyanzo vya maji, kupanda miti kwenye maeneo chakavu/nyika na ufugaji nyuki tangu mwaka 2008 hadi hivi leo, Lakini mwaka 2009 shirika la Umoja wa mataifa UNDP walitufadhili mradi wa kutoa elimu ya uhifadhi wa mazingira kwa wanajamii wa kata tatu Ludende, Mundindi na Milo katika wilaya ya Ludewa,  kuwatika miche ya miti Laki mbili na kutengeneza mizinga ipatayo 32; Mradi huu ulifanikiwa sana kwani tulifanikiwa kugawa miche takribani laki moja na elfu themanini kwa wanajamii wa Tarafa ya Mlangali, Liganga na Mawengi na Miche nyingine tuliwagawia wanachama wa Asasi ili kufanikisha zoezi zima upandaji miti na hivyo kuepusha ukame na kulinda mazingira. Kwahiyo katika sehemu hii ya uhifadhi wa mazingira kwa uhakika tumefanya vizuri kiasi cha kufikia nusu ya malengo ya miaka mitano tuliyojiwekea.

Asasi yetu pia imekuwa inafanya miradi ya utoaji elimu kwa jamii juu ya mada mbalimbali kama vile sera, utetezi na uhamasishaji, katika hili kwanza tulianza kufanya miradi ya Kisera hasa ile ya  utoaji wa Elimu  ya Haki ya mwanamke kumiliki Mali na Ardhi kwa ufadhili wa shirika la The Foundation For civil society (FCS) mwaka 2009; Hivyo kwa kuwa tulifanikiwa kufanya kazi nzuri na mfadhili huyu aliendelea kutufadhili kwa kila mradi ambao tuliomba kufanya hasa kwenye eneo hili la utoaji wa elimu kwa jamii pamoja na uhamasishaji juu ya haki ya mwanamke kumiliki Ardhi.  Kwa mara ya mwisho tulipata mradi mkubwa ambao bado unatekelezwa wa “Haki ya mwanamke kumiliki ardhi” ambao kimsingi utachukua miezi tisa kumalizika (utaisha Desemba 2012).

Hata hivyo tunakusudia kufanya vizuri kwa kila lengo tulilojiwekea ingawa kwa sasa tunaenda hatua kwa hatua na kuchukua lengo moja baada ya jingine  ili kuifikia jamii nzima ya Ludewa na kupunguza kero za wananchi ambazo ni vikwazo kwa maisha yao ya kila siku.

Huu mradi tuufanyao tunatarajia kufanya kwa mkoa mzima lakini kwa awamu kutegemeana na uwezo wa wafadhili kwa kila hatua kwani tamaduni zetu zinawatenga wanawake katika kumiliki mali na hasa mali ya ukweli ambayo ni Ardhi, na lengo letu ni kuondoa mfumo dume huo na kuleta usawa katika jamii nzima hasa katika umiliki wa ardhi, kwani pia  tunatambua msemo usemao  kuwa kumwelimisha mwanamke ni kuelimisha jamii nzima, na kwa mantiki hiyo kumkomboa mwanamke ni kuikomboa jamii nzima.

Mwisho

No comments: