KESI ya kuomba na
kupokea manufaa au rushwa inayomkabili mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya
Ludewa katika mkoa wa njombe Matei Felician Kongo upande wa mashtaka umemaliza
ushahidi wake.
Akifunga ushahidi wake
jana mbele ya hakimu makazi wa mahakama ya wilaya ya Ludewa Fredrick Lukuna
mwendesha mashtaka wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU)
Restuta Kessy akaiambia mahakama kuwa upande wa mashtaka umemaliza ushshidi
baada ya kuleta mashahidi wote waliotakiwa katika ushahidi huo.
Katika hali
iliyowashangaza wasikilizaji shahidi wa mwisho katika kesi hiyo ambaye anatajwa
kuwa rafiki mkubwa wa mshtakiwa Bw Aidani Luoga akaiambia mahakama kuwa machi
12 mwaka huu mshtakiwa alikwenda kwake kuomba namba ya akaunti ya NMB akampa
lakini akashangaa siku hiyo majira ya saa 9 mchana akakamatwa na takukuru.
Hata hivyo kabla ya
mahakama kutoa amri kama mwenyekiti huyo analo shtaka la kujibu au la wakili wa
mshtakiwa Frank Ngafumika akaiomba mahakama isifanye hivyo mpaka upande wa
utetezi utakapopewa nakala ya mwenendo wa kesi ili kujipanga kujibu hoja.
Awali ilidaiwa
mahakamani hapo kuwa kati ya oktoba mwaka jana na machi mwaka huu mshtakiwa
Matei Kongo aliomba rushwa kwa Samson
Mwaipugile mkazi wa Dar es Salaam ili aweze kumpa kwa upendeleo tenda ya ujenzi
wa barabara na kusambaza vifaa vya ofisi ikiwemo komputa katika halmashauri ya
wilaya ya Ludewa.
Mwenyekiti huyo wa
halmashauri ya wilaya ya Ludewa alikamatwa na kufikishwa mahakamani kwa madai
kuwa machi 12 mwaka huu alipokea rushwa ya shilingi laki moja (100,000) kwanjia
ya benki ya NMB Tawi la Ludewa kupitia
akaunti ya Aidan Luoga.
Kesi hiyo iliahirishwa
hadi Novemba 21 mwaka huu itakapokuja kupangwa tarehe ya kuanza kusikiliza
upande wa utetezi.
Katika kesi nyingine
Afisa mtendaji wa kijiji cha Kipangala katika Kata ya Luilo Ludewa katika mkoa
wa Njombe Bw Yohana Jenkin Pili jana alipandishwa kizimbani na taasisi ya
kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) kwa kushawishi na kutoa rushwa kwa
wananchi ili wasaini vocha hewa za pembejeo.
Pamoja naye
waliofikishwa mahakani hapo ni Kilian Kilian Mbawala ambaye ni mwenyekiti wa
kamati ya pembejeo ya kijiji cha kipangala na Bw Sebastian Haule ambaye alikuwa
wakala wa pembejeo katika kijiji hicho.
Akisoma hati ya
mashtaka mbele ya hakimu makazi wa wilaya ya Ludewa Fredrick Lukuna mwendeshs
mashtaka wa Takukuru Restuta Kessy akaimbia mahakama kuwa washtakiwa wote kwa
pamoja wanakabiliwa makosa 13.
KESSY washtakiwa wote
kwa pamoja walitenda makosa hayo mwezi
June mwaka huu ambapo waliwashawishi wananchi kupokea kila mmoja jumla
ya shilingi 20,000 kila mmoja ili wasaini vocha hewa kwa faida ya wakala
Sebastian Haule, makosa ambayo yanaangukia chini ya kifungu namba 15 cha sheria
ya kuzuia na kupambana na rushwa no 11/2007.
Washtakiwa walikana
kuhusika na makosa yote yanayowakabili na kdhaminiwa kwa kiasi cha shilingi
milioni moja kila mmoja.
Kesi itakuja kwa kusikilizwa oktoba 21 mwaka huu na
upelelezi wa kesi hiyo umekamilika.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment