Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

July 10, 2014

FILIKUNJOMBE AWABANA MAKANDARASI WILAYANI LUDEWA





 Filikunjombe akipata maelezo kutoka kwa mtaalam wa TANROAD


              Mkurugenzi wa GS CONTRUCTORS CO.LTD akipokea mkataba

Mbunge wa jimbo la Ludewa katika mkoa wa Njombe Deo Filikunjombe ameanza kuwabana Makandarasi wanaofanya upanuzi wa barabara ya  Itoni,Mkiu,Liganga na ile ya Mkiu,Ludewa hadi Nchuchuma kwa kufanya ukaguzi wa kushitukiza ili kubaini changamoto wanazokabiliana nazo.

Katika ukaguzi huo aliweza kujionea baadhi ya makandarasi ambao wanafanya vizuri na kwenda na muda waliopangiwa katika mkataba na wengine kushindwa kufanya kazi kwa wakati kutokana na uchakavu wa mitambo wanayoitumia hali ambayo iliwafanya kushindwa kujitetea walipotakiwa kujieleza kwanini hali imekuwa tofauti na mkataba.

Barabara hizo zinajengwa kwa gharama ya shilingi 7.8 bilioni ambazo katika mkataba makandarasi walipewa muda wa mienzi miwili kufanya upanuzi huo ili mitambo ya wawekezaji wa miradi ya makaa ya mawe  Nchuchuma na chuma cha Liganga zinatakiwa kuisha mapema ili kuleta chachu ya maendeleo wialayani Ludewa.

Barabara hizo ni zile za Itoni Mlangali ambayo amepewa Boimanda modern CO.LTD,Mlangali hadi Ludewa inajengwa na Mtwivila Traders Contruction CO.LTD,Ludewa hadi Ngomang'ombe,Mchuchuma inajengwa na G;S Contractors CO.LTD na ile ya Mkiu hadi Liganga inajengwa Canopies International(T)LTD. 

  Filikunjombe amewaonya na kuwataka makandarasi wazarendo wanaofanya kazi ya kupanuzi wa barabara ya Itoni hadi Ludewa kuwa waaminifu na waadilifu vinginevyo hatasita kuomba mwongozo wa spika kwa yeyote atakayekwenda kinyume na mkataba.

Filikunjombe aliwataka Makandarasi hao kufanya kazi kama walivyosaini mikataba yao ili kujiletea sifa kwa makandarasi wazawa kwani kwa kufanya hivyo wanaweza kuaminiwa na Serikali yao hali ambayo itawasaidia kupata tenda nyingi nchini na kuweza kujitangaza zaidi.

“mimi nawahakikishieni kuwa kazi hii ya Ludewa inaweza kuwapa sifa kubwa mkiifanya vizuri na inaweza ikawaweka pabaya kama mtashindwa kuifanya kwa kiwango kinachokubalika hivyo wananchi wa Ludewa hawata kubali kuona fedha za Serikali hazifanyi kazi iliyopangwa ninawaomba ifanyike kwa muda uluiopangwa”,alisema Filikunjombe.

Alisema wilaya ya Ludewa inachangamoto kubwa ya miundombinu hali inayowafanya vijana kukimbilia mjini kwa lengo la kuatafuta amaisha lakini kwa kasi hii ya Serikali inayoongozwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete vijana walio wengi wataweza kurudi na kuishi wilayani hapa.

Aidha mkurugenzi wa G,S Contructors Bw.Seven Gamba ambaye kampuni yake inakarabati barabara ya Ludewa mjini hadi Nchuchuma alimsifu Filikunjombe kwa ufuatiliaji wake kwani kwa kufanya hivyo wakandarasi wazawa watafanya kazi kwa umakini mkubwa tofauti na zamani walikuwa wakibweteka.

Bw.Gama alisema licha ya mitambo yake kuwa mibovu mara kwa mara lakini amejifunza kitu kikubwa kutoka kwa filikunjombe ambacho kinahitaji utekelezaji wa haraka hivyo atajitahidi kuimaliza kazi kwa muda uliopangwa ili kuweza kujizolea sifa ambazo zitamsaidia kupata kazi kubwa zaidi.

Aliwataka makandarasi wengine kufanya kazi kwa juhudi na uaminifu mkubwa kama alivyowaelekeza Filikunjombe kwani mbunge huyo anania nzuri na makandarasi wanaofanya kazi katika wilaya ya Ludewa ambao mpaka sasa baadhi wako katika hatua nzuri ya utendaji kazi.

Mwisho.

No comments: