Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

March 11, 2016

MBUNGE WA JIMBO LA LUDEWA DEO NGALAWA ATOA SHILINGI MILIONI TANO KANISA LA LUTHERANI LUDEWA MJINI.

 Mh.Deo Ngalawa akifanyiwa maombezi maalum

Bw.Lusiano Mbosa akimshukuru Mh.Ngalawa kwa msaada wake wa shilingi milion tano
 Mh.Deo Ngalawa akifanyiwa maombezi maalum
  Mh.Deo Ngalawa akifanyiwa maombezi maalum
hizi ndizo nyumba za wachungaji ambazo Mh.Ngalawa alichangia fedha ya ukarabati kiasi cha shilingi milioni mbili

Mh.Deo Ngalawa akiongea na waumini wa kanisa la Lutherani Ludewa mjini


Mh.Deo Ngalawa akiongea na waumini wa kanisa la Lutherani Ludewa mjini

Mbunge wa jimbo la Ludewa katika mkoa wa Njombe Mh.Deo Ngalawa ametoa mchango wa shilingi milioni tano katika Kanisa la Kiluteli Ludewa Mjini,fedha hizo milioni mbili ni ukarabati wa nyumba mbili za wachungaji na milioni tatu ni mchango wa gari ambayo inatakiwa kusaidia huduma za kichungaji katika Kanisa hilo wilayani Ludewa.


Akitoa fedha hizo katika maombezi maalumu yaliyofanywa na Kanisa hilo ili kumuombea mbunge huyo kufanya kazi kwa ufanisi Mh.Ngalawa alisema kuwa wilaya ya Ludewa inahitaji watu wanaoweza kubuni miradi ambayo itaweza kuwakwamua waumini wa dini mbalimbali kiuchumi hivyo ni vema wachungaji wakaanza kutoa elimu hiyo kwa waumini wao.


Mh.Ngalawa alisema kuwa Kanisa hilo limeonesha kuwa linamipango mizuri ya kujitegemea kutokana na hali halisi ambayo imeonesha katika mishango inayotolewa na kila muumini siku ya ibada hivyo yuko tayari kuwaunga mkono wale wote wenye malengo ya kuibua miradi katika vikundi mbalimbali.


Alisema kuwa kasi ya kimaendeleo wilayani Ludewa bado iko nyuma kutokana na ugumu wa maisha unaowakabili wananchi wa wilaya ya Ludewa hiyo ndiyo sababu ya mtangulizi wake hayati Deo Filikunjombe enzi za uhai wake alikuwa mkali sana Bungeni na alisimamia ukweli kwa maslahi ya wanaLudewa hivyo kila mwananchi wa jimbo hili anapaswa kukaza buti katika kuharakisha maendeleo mingoni mwa jamii.


“Nimeupenda mfumo wenu wa kuchangishana fedha kwa uchache wenu mumeweza kuzijenga nyumba hizi za wachungaji hivyo nami nawaunga mkono kwa kutoa shilingi milioni mbili katika ukarabati pia natoa milioni tatu ili kuharakisha ununuzi wa kari ya mchungaji ambayo itamsaidia kutoa huduma maeneo mbalimbali ya wilaya yetu”,alisema Mh.Ngalawa.


Mh.Ngalawa aliwataka washirika wa makanisa na Dini nyingine wilayani hapa kuiga mfano huo ambao unamalengo mazuri ambayo wisho wa siku itakuwa ni chachu ya kimaendeleo kwa wilaya nzima kwani unafundisha namna ya kujitegemea na kuachana na wafadhiri ambao hutoa fedha zao zikiambatana na masharti magumu.


Akishukuru kwa msaada huo kwa niamba ya waumini wa Kanisa hilo ambaye pia ni mzee wa Kanisa la Kirutheli wilayani Ludewa Bw.Lusiano Mbosa alisema kuwa Kanisa hilo linampango wa kujenga nyumba ya wageni ili kujiingizia kipato hivyo huo ni mwanzo tu wa safari yao ya kujitegemea.


Mwisho.


No comments: