Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

February 23, 2016

WANANCHI LUDEWA WAFANYA UFUGAJI WA SAMAKI NA KILIMO CHA MATUNDA IKIWA NI MAANDALIZI YA MIRADI YA CHUMA NA MAKAA YA MAWE.

Hili ni shamba moja wapo la migomba linalopatikana Mundindi wilayani Ludewa


 Haya ni baadhi ya mabwawa ya Samaki yaliyoko Mundindi wilayani Ludewa

 Aina ya ndizi zilizopo Mundindi wilaya Ludewa

 Aina ya ndizi ambazo hulimwa nchini Mexico sasa zinapatikana Mundindi wilayani Ludewa



 miembea na maembe makubwa yanayofikia kilo mbili yanapatikana Mundindi wilayani Ludewa


 bwawa la samaki aina ya  Sato
 Nguruwe wa Kisasa walioko Mundindi

mbegu ya ndizi kutoka Mexico





Wananchi wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe wameanza maandalizi ya ufugaji wa samaki na kilimo cha matunda mbalimbali kwaajili ya wawekezaji ambao wanaotarajia kuja wilayani hapa kufanya kazi katika migodi ya chuma cha Liganga na Makaa yam awe Nchuchuma miradi ambayo imekuwa ikitajwa kila kipindi cha kampeni za uchaguzi mkuu na bila utekelezaji.


Akiongea na mwandishi wa habari hizi katika kijiji cha Mundindi wilayani Ludewa Padre Melodious Mlowe ambaye ndio mfao wa wakulima na wafugaji wilayani hapa alisema kuwa ili kujiandaa na uwekezaji wananchi wanapaswa kuandaa mashamba yao na ufugaji wa kisasa bila kujali miradi hiyo inatarajia kutekelezeka lini.


Padre Mlowe alisema kuwa yeye ameshajiandaa kwani mpaka sasa ameshafungua mashamba ya matunda mbalimbali yakiwemo machungwa,maembe,Parachichi hufikia uzito wa kilogram tatu na ndizi kutoka vyuo vya utafiti wa kilimo vya ndani ya nchi na nje ya nchi ambayo kwa kiasi kikubwa yameshaanza kupata soko katika maeneo mbalimbali ndani ya mkoa na nje ya mkoa.


Alisema kuwa anazaidi ya hekali 20 za matunda  ambapo kwa upande wa ndizi kuna migomba ambayo aliitoa mashamba ya kilimo ya Serikali Bihalamulo,chuo cha kilimo SUA  Morogoro,Ruanda na Burundi ambayo ni aina maalumu na inazalisha kwa wingi pia kuna migomba ambayo inazaa ndizi za mapambo lakini zinaliwa kama kawaida kutoka nchini Mexico.


Kwa upande wa Parachichi ana aina ambayo aliitoa nchini India pia michungwa na miembe ambayo aliitoa katika chuo cha SUA ikiwa ni malengo yake ya kuwagawia wananchi ili waweze kufanya kilimo cha matunda hayo ili kuweza kuwalisha wageni ambao wataajiliwa katika miradi hiyo miwili mikubwa inayotarajia kuanza.


“Nimefungua mashamba makubwa na kutafuta mbegu zilizofanyiwa utafiti ili kuisaidia jamii ya wilaya ya Ludewa kuanza kujiandaa na fulsa kwani baadhi ya wananchi wanafikiri miradi hiyo itaweza kuwaajiri wananchi wote jambo ambalo sio sahihi hivyo lazima kila mtu ajifunze kuzalisha kwa wingi ili itakapoanza miradi hiyo aweze kujipatia kipato kwa kuwauzia wafanyakazi wa miradi hii”,alisema Padre Mlowe.


Padre Mlowe licha ya kilimo cha matunda pia alisema kuwa ameweza kutengeneza mabwawa ya samaki zaidi ya 25 ambayo yana samaki aina mbalimbali wakiwemo Sato na Pelege wa bwawa la Mtela ambao tayari amekwishaanza kuwauzia raia wa China ambao wanaendelea na maandalizi ya ujenzi wa viwanda katika migodi hiyo.


Alisema kuwa ufugaji wa Samaki huo aliupata kutoka kwa watafiti wa samaki kutoka Mwanza hivyo kila Bwawa linaaina yake ya Samaki kwa mwishoni wa mwa ka 2015 aliweza kuwavua samaki na kuwagawia wananchi ili kuonja radha ya samakini hao ikiwa ni moja ya ushawishi kwa wananchi ili waweze kujifunza ufugaji wa samaki hao ambao wanaweza kuwa ni ukombozi mkubwa katika uchumi wao.


Vilevile katika shamba hilo ambalo ni la mfano wilayani Ludewa kuna ufugaji wa Bata,Kuku,Ng’ombe wa maziwa pamoja na Nguruwe kwani wawekezaji wa kichina hupendelea vyakula hivyo ambapo ufugaji wake hautumii gharama kubwa kwani kuna baadhi ya wananchi wameweza kufika katika shamba lake na tayari wameanza ufugaji huo pamoja na kilimo cha matunda.


Aidha aliwataka wananchi wa wilaya ya Ludewa kuendelea kujiandaa kuzalisha katika uwingi bila kujali maneno ya kukatishwa tamaa kuwa miradi hiyo ya Chuma na Makaa ya mawe ni hadhithi tu haiwezi tokea.


Mmoja wa wananchi wa wilaya ya Ludewa Bw.Albetho Mwinuka alisema kuwa wananchi wa wilaya ya Ludewa ni watendaji wazuri wa kazi lakini wamekuwa wakikatishwa tamaa na Serikali kutokana na kushelewa kuanza miradi hiyo mikubwa ambayo ingeweza kuinua uchumi wa Taifa.


Mwisho.

No comments: